Mkuu wa Wilaya ya Iramba mkoani Singida Suleiman Mwenda akitoa maelekezo kwa wajumbe wa kamati ya Siasa na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama wa wilaya hiyo wakati wakikagua moja ya caravati linalojengwa katika Barabara ya Maluga Mtaa Saba -Misuna na Mgungia hadi Kaselya wakati kamati hizo zilipokuwa zikikagua miradi ya maendeleo iliyotekelezwa na Rais Samia Suluhu Hassan katika kipindi cha mwaka mmoja wa uongozi wake Tarafa ya Shelui wilayani humo jana.
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Iramba, Samuel Ashery akizungumza wakati kamati hizo zilipokuwa zikikagua mradi wa maji wa Kijiji cha Wembere uliopo katika Tarafa hiyo.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Innocent Msengi akizungumza kwenye ziara hiyo.
Afisa Tarafa ya Kinampanda Cholo Mtaki akiwatambulisha viongozi katika mkutano wa hadhara uliofanyika Kijiji cha Kitukutu wakati wa ziara ya kamati hizo.
Meneja wa Wakala wa Majisafi na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) Wilaya ya Iramba Mhandisi Ezra Mwacha akitoa taarifa ya ujenzi wa mradi wa maji wa Kijiji cha Wembere.
Mganga Mfawidhi wa Zahanati ya Misigiri akitoa taarifa ya mradi wa vyoo na uwekaji wa miundombinu ya maji katika zahanati hiyo.
Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Kitukutu Dada Kazimoto akizungumza mbele ya kamati hiyo.
Ukaguzi wa tenki la maji katika zahanati hiyo ukifanyika.
Diwani wa Kata ya Ulemo akichangia jambo kwenye ukaguzi wa mradi huo wa vyoo.
Mganga Mfawidhi wa Zahanati ya Ulemo Luka Kasanga akitoa taarifa ya ujenzi wa zahanati hiyo.
Muonekano wa zahanati hiyo.
Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda akichangia jambo wakati wa ukaguzi wa ujenzi wa zahanati hiyo ya Ulemo.
Muonekano wa bweni la Wasichana wa Shule ya Sekondari ya Tumaini baada ya ujenzi wake kukamilika
Wajumbe wa kamati hizo wakipokea taarifa kutoka kwa Mkuu wa Shule ya Wasichana ya Tumaini, Mwalimu Zainabu Mtinda ya kukamilika kwa ujenzi wa bweni katika shule hiyo.
Mkuu wa Shule ya Sekondari ya KengyegeMwalimu Emmanuel Twiyogehe akitoa taarifa ya ujenzi wa shule mpya ya Sekondari ya Maluga.
Muonekano wa baadhi ya majengo yanayoendelea kujengwa Shule mpya ya Maluga.
Mafundi wakiendelea na ujenzi wa shule hiyo mpya ya Maluga.
|
Mkzi wa Kijiji cha Maluga akiishukuru Serikali na Rais Samia Suluhu Hassan kwa ujenzi wa shule hiyo. |
Diwani wa Kata ya Maluga akichangia jambo kuhusu ujenzi wa shule hiyo.
Wajumbe wa kamati hizo wakikagua ujenzi wa shule hiyo.
Mafundi wakiendelea na ujenzi wa shule hiyo.
Mkutano wa hadhara ukiendelea Kijiji cha Kitukutu.
Mkutano ukiendelea.
Katibu Mwenezi wa CCM Wilaya ya Iramba Michael Abbas akizungumza wakati akiwatambulisha viongozi wa chama hicho kwenye mkutano huo.
Katibu wa CCM wa Wilaya ya Iramba, Comrade Ephrahimu Kolimba akizungumza kwenye mkutano huo.
Afisa Elimu Sekondari wa Wilaya hiyo Mr Mwajala akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya hiyo ambapo aliwahimiza Wazazi na Walezi kuhamasika kuchangia chakula cha wanafunzi wakiwa shuleni.
Mkaguzi wa mradi wa maji wa Kijiji cha Wembere ukifanyika.
Muonekano wa mradi huo wa maji wa Kijiji cha Wembere.
Mwenyekiti wa Kijiji cha Wembere Eliud Mbogo akiishukuru Serikalikwa kuwapelekea mradi huo.
DC Mwenda akizungumza wakati wa ukaguzi wa mradi huo wa maji.
Makofi yakipigwa kufurahia mradi huo.
Ukaguzi wa ujenzi wa Kituocha Afya cha Umtoa ukiendelea.
Muonekano wa baadhi ya majengo yanayoendelea kujengwa ya Kituocha Afya Mtoa
Mganga Mkuu Mfawidhi wa Kituo cha Afya Mtoa, Sori Abushehe akitoa taarifa ya ujenzi wa kituo hicho.
Muonekano wa chumba cha maabara ya Shule ya Sekondari ya Mtoa kinachoendelea kujengwa.
Ukaguzi wa ujenzi wa maabara hiyo ukiendelea
Meneja wa TARURA wa wilaya hiyo Venance Kibona akitoa taarifa ya ujenzi wa Barabara ya Shelui kwenda Tintigulu.
DC Mwenda akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Nselembwe wakati wa ukaguzi wa barabara hiyo.
Mkuu wa Wilaya ya Iramba Suleiman Mwenda pamoja na wajumbe wa kamati hizo wakisaidia kuchanganya mchanga wa ujenzi wa nyumba ya watumishi wa Kituo cha Afya Shelui.
Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya cha Shelui, Alex Mpwenku akitoa Taarifa ya ujenzi wa nyumba ya watumishi wa kituo hicho.