Sunday, July 31, 2022
WANANCHI WAZUIA MSAFARA WA WAZIRI WA MAJI, WALIA KERO YA MAJI
Saturday, July 30, 2022
WAZIRI AWESO ATAKA MABONDE YA MAJI KWENDA KUJIFUNZA BONDE LA KATI UFANISI WA UTENDAJI KAZI
Waziri wa Maji Jumaa Aweso (katikati) akikata utepe kuashiria uzinduzi wa mradi wa wa ujenzi wa ofisi ya maabara ya bodi ya maji Bonde la Kati, mjini Singida leo Julai, 30, 2022. Kutoka kulia ni Mstahiki Meya wa Manispaa ya Singida, Yagi Kiaratu, Afisa wa Bodi ya Maji Bonde la Kati, Mhandisi Danford Samson, Mkuu wa Wilaya ya Singida, Mhandisi Paskas Mulagiri, Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Singida, Lusia Mwiru na Mjumbe wa Siasa Mkoa wa Singida, Diana Chilolo.
Mkurugenzi wa Rasilimali za Maji Nchini Dk. George Lugomela akitoa taarifa ya mradi huo.Waziri wa Maji Jumaa Aweso akizindua jengohilo lililopo Kata ya Utemini mjini Singida.
Mwenyekiti wa Bodi ya Maji Taifa, Mhandisi Mbogo Futakamba akizungumza kwenye hafla hiyo.
Mwenyekiti wa Bodi ya Maji Bonde la Kati, William Mabula akizungumza kwenye hafla hiyo.
Waziri wa Maji Juma Aweso (katikati) akitoka kukagua maabara ya maji.
Kwaya ya Chuo cha Utumishi wa Umma Mkoa wa Singida ikitoa burudani.
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Singida, Yagi Kiaratu, akizungumza kwenye uzinduzi huo.Mjumbe wa Siasa Mkoa wa Singida, Diana Chilolo. akizungumza kweny hafla hiyo kwa niaba ya mwenyekiti wa chama hicho Mkoa wa Singida.
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Singida, Lusia Mwiru , akichangia jambo kwenye hafla hiyo.
Mkuu wa Wilaya ya Singida, Mhandisi Paskas Mulagiri akizungumza kwenye hafla hiyo.Mwenyekiti wa Bodi ya Maji Bonde la Kati aliyemaliza muda wake. Mhandisi Samson Mabala akizungumza kwenye hafla.
Wajumbe wa Bodi ya Maji Bonde la Kati waliomaliza muda wao wakiwa kwenye hafla hiyo.
Friday, July 29, 2022
MREMA ATOA NENO UTEUZI WAKUU WA MIKOA ULIOFANYWA NA RAIS SAMIA
Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha TLP, Augustino Mrema.
Na Thobias Mwanakatwe
MWENYEKITI wa Taifa wa Chama cha TLP, Augustino Mrema, amesema uteuzi na
mabadiliko ya wakuu wa mikoa uliofanya na Rais
Samia Suluhu Hassan iwe chachu kwa walioteuliwa kufanya kazi kwa bidii
kumsaidia rais katika kuleta maendeleo makubwa ya kiuchumi nchini.
Akizungumza jana kwa simu akiwa jijini Dar es Salaam, alisema rais
anapofanya mabadiliko ya viongozi dhamira yake kuu ni kutaka kuona wasaidizi
wake wanamsaidia katika kuleta maendeleo kwa wananchi.
Mrema ambaye ni mwanasiasa mkongwe ambaye amewahi kushika nyadhifa kadhaa
ikiwano ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, alisema rais
tuliyenaye anapenda kuona wasaidizi wake wanaleta mabadiliko ya kimaendeleo
katika maeneo aliyowateua.
"Viongozi waliobahatika kuteuliwa cha msingi wakishaanza kutekeleza
majukumu yao wachape kazi kuwaletea maendeleo wananchi maana dhamira ya rais ni
kuiona Tanzania inakuwa nchi yenye watu wake wenye maendeleo makubwa,"
alisema Mrema.
Mrema aliongeza kuwa mara nyingi watu wanapoteuliwa kushika nyadhifa
mbalimbali za uongozi wanafurahia badala ya kwenda kufurahia unapokuwa
umesaidia kuleta mabadiliko ya maendeleo kwenye eneo ulilopangiwa.
Alisema walioachwa katika uteuzi huu hawana sababu ya kujisikia wanyonge
kwani mchango wao walioutoa wakiwa viongozi unatambulika kwani uongozi ni
kupokezana vijiti.
"Mimi nilikuwa Waziri wa Mambo ya Ndani leo hii si niko benchi nafasi
ameishika mwingine, na kwenye hizi kazi ukifanya vizuri utakumbukwa daima kwa
uwajibikaji uliotukuka na heshima utakuwa nayo mbele ya jamii kama ikivyo
kwangu mimi," alisema Mrema.
Mrema alisema moja ya majukumu ya Mkuu wa mkoa ni pamoja na kuhakikisha
mkoa wako unakuwa na makusanyo ya mapato na kuzuia rushwa na upotevu wa mapato
kwenye halmashauri zilizopo kwenye mkoa husika.
Aliongeza kuwa katika siku za karibu tumekuwa tukishuhudia na hata katika
ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) halmashauri
nyingi zikikumbwa na kashfa ya ubadhirifu wa mapato na wakuu wa mikoa wapo
lakini hawachukui hatua kwa watendaji wao wa chini.
Mrema alisema sio jambo lenye afya kiongozi wa kitaifa anapofanya ziara
katika mkoa wako na kuibua suala la ubadhirifu wa mapato wakati wewe kama Mkuu
wa Mkoa upo na haukufanya jambo lolote kuchukua hatua kudhibiti haki hiyo.
MADEREVA BAJAJ, BODABODA KUWA MABALOZI WA TANESCO SINGIDA
Thursday, July 28, 2022
SERIKALI, LIONS CLUB YAKABIDHI CHUO CHA UFUNDI MSANDAKA MKOANI KILIMANJARO
WAZAZI WATAKIWA KUHAKIKISHA WATOTO WENYE ULEMAVU WANAHESABIWA
Wednesday, July 27, 2022
DK. MWIGULU: UJENZI WA MIRADI YA BARABARA ILINGANE NA THAMANI YA FEDHA ZINAZOTOLEWA
Mkuu wa Mkoa wa Singida Dk. Binilith Mahenge ambaye alikuwa Mwenyekiti akiongoza kikao hicho
Tuesday, July 26, 2022
TFRA YATOA WITO KWA WAKULIMA KUJISAJILI ILI WANUFAIKE NA RUZUKU YA SERIKALI.
Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania –TFRA Dkt Stephan Ngailo akizungumza na wanahabari jijini Dar es salaam akitoa taarifa ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluh Hassan kuzindua mpango wa utoaji wa ruzuku ya mbolea kwa wakulima.
……………………….
NA MUSSA KHALID
Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania -TFRA imewataka wakulima nchini kujitokeza kujiandikisha na kujisajili kwenye Ofisi za serikali za vijiji vyao ili waweze kunufaika na mpango wa serikali wa kuwapunguzia makali ya bei ya Mbolea kupitia Ruzuku.
Kauli hiyo imetolewa jijini Dar es salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa TFRA Dkt Stephan Ngailo wakati akitoa taarifa ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluh Hassan kuzindua mpango wa utoaji wa ruzuku ya mbolea kwa wakulima.
Dkt Ngailo amesema kutokana na kupanda kwa bei za mbolea katika soko la Dunia na hapa nchini serikali imetenga kiasi cha Shilingi Bilioni 150 kugharamia ruzuku ya mbolea itakayotolewa kwa wakulima wote nchini kwa lengo la kupunguza makali ya bei za mbolea na kuongeza uzalishaji na tija katika kilimo.
Amesema kuwa Serikali imeamua kutumia Mfumo wa kidigitali kutekeleza mpango wa ruzuku ya Mbolea ili kuongeza ufanisi,kupunguza mianya ya udanganyifu Pamoja na Muda na gharama za Usimamizi.
Aidha Dkt Ngailo amesema kuwa Mbolea zitakazohusika kwenye Ruzuku ni za kupandia na kukuzia ambapo DAP kwa ajili ya kupandia na Urea kwa kukuzia ambazo zote ni takriban Asilimia 50 ya matumizi yote ya Mbolea Nchini.
Dkt Ngailo ameeleza kuwa Mfumo huo utafanya kazi kwa mkulima aliyesajiliwa ataenda kwa mfanyabiashara wa Mbolea aliyesajiliwa Kwa ajili ya kununua Mbolea na kuonyesha namba ya utambulishe aliyopewa wakati wa usajili.
“Ili kuhamasisha matumizi ya Mbolea zinazozalishwa nchini,zinazozalishwa na viwanda vya ndani zitaingia kwenye mpango wa ruzuku kulingana na mahitaji ya soko”amesema Dkt Ngailo
Amesema uuzaji wa mbolea kwa wakulima na malipo ya ruzuku ya mbolea mfumo huo utafanya na makampuni yataingiza na kuzalisha mbolea nchini na kuifungasha katika mifuko yenye uzito wa kilo 25 na 50 ambayo itaandikwa ‘MBOLEA YA RUZUKU’na itachapwa QR Code itakayotolewa na TFRA.
Amesema utekelezaji wa mpango wa ruzuku ya Mbolea utahusisha wadau mbalimbali wakiwemo Wizara ya Kilimo,Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea TFRA,Kamati Tendaji ya Ruzuku,Sekratieti za mikoa,Mamlaka ya serikali za mitaa,WAINGIZAJI/wazalishaji wa Mbolea,Mawakala wa Mbolea,Taasisi za Fedha na wakulima.
Pia ameziomba serikali za vijiji,viongozi,watendaji na mabalozi sambamba na maafisa ugani kushiriki kikamilifu katika zoezi la usajili wa wakulima na utoaji wa ruzuku ili kuhakikiha mkulima anafaida jambo litakaloisaidia kukuza uchumi wanchi
TANESCO SINGIDA YAANZISHA UTARATIBU WA KUWASIKILIZA WANANCHI ILI KUJUA CHANGAMOTO ZAO KUHUSU UMEME
Afisa Uhusiano na Huduma kwa Wateja wa Tanesco Mkoa wa Singida, Rehema Mwaipopo akizungumzia huduma mpya ya maombi ya kuunganishiwa umeme kwa njia ya mtandao iitwayo NIKONEKT ambayo inafanyika kwa kutumia simu ambapo muombaji anaomba akiwa nyumbani bila ya kufika ofisi za shirika hilo.
Monday, July 25, 2022
KAMATI YA SENSA MKOA WA SINGIDA YAWATEMBEA WAKUFUNZI 216 WATAKAO HITIMU MAFUNZO KESHO
Mratibu wa Sensa Mkoa wa Singida, Naing'oya Kipuyo, akizungumza wakati Wajumbe wa Kamati ya Sensa ya Watu na Makazi mkoani hapa walipowatembelea leo Julai 25, 2922 Wakufunzi wa Makarani wa Sensa wanaotarajiwa kuhitimu kesho Julai 26, 2022 katika ukumbi wa VETA mjini hapa ambapo Mkuu wa Mkoa wa Singida Dk.Binilith Mahenge anarajiwa kuwa mgeni rasmi.
OFISI YA ARDHI MKOA WA SINGIDA YAANZA KUSIKILIZA KERO ZA MIGOGORO YA ARDHI
Kamishna wa Ardhi Msaidizi Mkoa wa Singida, Shamim Hoza akizungumzia kuhusu ofisi ya Ardhi Mkoa wa Singida ilivyoanza leo Julai 25,2022 kusikiliza kero za migogoro ya ardhi ya wananchi kwa kila halmashauri ili ziweze kutatuliwa.