Thursday, December 29, 2022

REA YAZINDUA MRADI WA KUSAMBAZA UMEME MAENEO YA VIJIJI MIJI SINGIDA, MKANDARASI AKABIDHIWA RASMI MBELE YA DC

 Mkuu wa Wilaya ya Singida Mhandisi Paskas Muragili (katikati) kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Singida akiwasha kifaa maalumu cha kupiga king'ora kuashiria uzinduzi rasmi wa mradi mpya wa kusambaza umeme kwenye Vijiji Miji viliyopo pembezoni mwa Manispaa ya Singida katika hafla iliyofanyika Kata ya Mwankoko Desemba 29,2022 ambao utagharimu Sh. 7.11 Bilioni zilizotolewa na Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) amapo  Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) litakuwa msimamizi wa mradi huo. 

Na Dotto Mwaibale, Singida

SERIKALI kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imezindua mradi mpya wa kusambaza umeme kwenye Vijiji Miji viliyopo pembezoni mwa Manispaa ya Singida ambao utagharimu Sh. 7.11 Bilioni na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) litakuwa msimamizi wa mradi huo.

Mradi huo wa kusambaza umeme katika Vijiji Miji (Peri-urban Electrification)  ambao umezinduliwa Desemba 29, 2022 Kitongoji cha Kitope Darajani Kata ya Mwankoko utatekelezwa kwenye vitongoji 34 vilivyopo katika  Kata 9 ambapo wateja watarajiwa ni zaidi ya 2000.

Akizindua Mradi huo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mkuu wa Wilaya ya Singida Mhandisi Paskas Muragili aliwaomba wananchi wachangamkie mradi huo kwa kuanza kusuka  nyaya za umeme katika nyumba zao ili waweze kufungukiwa kwa gharama ya Sh.27,000.

"Mradi huu ukikamilika unakwenda kubadilisha uchumi wa wanananchi kwani watautumia umeme huo kuanzisha viwanda vidogo  na shughuli zingine za uzalishaji ambazo zitatumia nishati hiyo hivyo kuinua uchumi wa mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla" alisema Muragili.

Muragili alimuomba mkandarasi wa mradi huo kuukamilisha ndani ya mwaka mmoja badala ya miezi 18 aliyopewa  kuukamilisha kwa sababu hakuna sababu yoyote ya kuchelewa kuukamilisha ndani ya muda huo kwa kuwa unatekelezwa kwenye maeneo yenye miundombinu mizuri ya barabara.

Akifafanua kuhusu Mradi huo, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Nicolaus Moshi  alisema mradi wa usambazaji nishati ya umeme katika maeneo yaliyo pembezoni mwa miji kwa hapa nchini Mkoa wa Singida ndio wanaupata kwa mara ya kwanza.

Alisema mradi huo utajenga jumla ya kilomita 40.5 za msongo wa kati na msongo mdogo na kupitia mradi huo watafunga mashine umba au Transfomer 33 katika vitongoji vilivyotajwa na kuweza kuwaunganishia wateja wa awali 1802 ambapo aliwaomba wananchi wa maeneo utakapo pita mradi huo kuchangamkia fursa hiyo.

Moshi alisema REA imekuwa ikitekeleza miradi mingine mingi hapa nchini Mkoa wa Singida ukiwa ni moja ya mikoa ambayo inanufaika na miradi hiyo na akatumia nafasi hiyo kumtambulisha kwa wananchi na mgeni rasmi Mkandarasi wa Kampuni ya  Central Electricals International Ltd anayetekeleza mradi huo na kukabidhiwa rasmi mbele ya mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Singida, Mhandisi Paskas Muragili ili aanze kufanya kazi .

Katika hafla hiyo viongozi mbalimbali walipata fursa ya kutoa salamu huku wakimshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha za kutekeleza mradi huo na mingine mingi na wito wao mkubwa wakiomba wananchi kutunza miundombinu ya mradi huo na kuwataka wachangamkie umeme huo kwa kuanzisha miradi ya kuinua uchumi wao.

Baadhi ya viongozi waliopata fursa ya kutoa salamu ni Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Singida, Lusia Mwiru, Diwani wa Kata ya Mwankoko, Emmanuel Daniel, Mbunge wa Singida Mjini ambaye aliwakilishwa na Diwani wa Kata ya Kisaki, Moses Ikaku, Mwenyekiti wa Kijiji cha Mwankoko (A) Jacobo Yohana na  Mstahiki Meya wa Manispaa ya Singida, Yagi Kiaratu.

 Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Nicolaus Moshi (kulia) akimkabidhi faili la mkataba wa utekelezaji wa mradi huo, Meneja Mradi wa Kampuni ya Central Electricals International Ltd,  Pravin Thorat inayo jenga mradi huo. Katikati anayeshuhudia tukio hilo ni Mwakilishi wa Mbunge wa Singida Mjini, Diwani wa Kata ya Kisaki, Moses Ikaku.
 Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Nicolaus Moshi (kulia) akimkabidhi faili la mkataba wa utekelezaji wa mradi huo, Meneja wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Mkoa wa Singida, Mhandisi Florence Mwakasege.
Picha ya pamoja baada ya kukabidhiana mkataba huo.
 Wafanyakazi wa Kampuni ya Central Electricals International Ltd wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa hafla hiyo.
Wazee wa Kata ya Mwankoko wakiwa kwenye hafla hiyo.ya uzinduzi wa mradi huo.
Hafla hiyo ikiendelea.
Wanawake wakisrebuka kwenye hafla hiyo
Uzinduzi wa mradi huo ukiendelea.
Wananchi wakiwa na furaha katika uzinduzi huo.
Uzinduzi ukiendelea.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Mwankoko (A) Jacobo Yohana akizungumza. 

 Diwani wa Kata ya Mwankoko, Emmanuel Daniel, akizungumza.
 Diwani wa Kata ya Kisaki, Moses Ikaku, akizungumza kwa niaba ya Mbunge wa Jimbo la Singida mjini.
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Singida, Yagi Kiaratu akizungumza.
nMwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Singida, Lusia Mwiru, akizungumza.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Nicolaus Moshi, akizungumza wakati akitoa taarifa ya utekelezaji wa mradi huo.


Wafanyakazi wa kampuni inayotekeleza mradi huo wakijitambulisha.
Mkuu wa Wilaya ya Singida Mhandisi Paskas Muragili, akipeana mkono na Meneja Miradi wa  Kampuni ya Central Electricals International Ltd,  Pravin Thorat wakati wa uzinduzi huo.

Viongozi wakiwa meza kuu wakati wa uzinduzi wa mradi huo.
Picha ya pamoja na mgeni rasmi.
Picha ya pamoja.
Picha ya pamoja na mgeni rasmi
 

Tuesday, December 27, 2022

KANISA LA ABC LATOA NGUO, MCHELE KWA WAJANE, WAGANE JIJINI DAR ES SALAAM

 Askofu Mkuu wa Kanisa la ABC Tanzania lililopo Mtaa wa Mandela jijini Dar es Salaam, Flaston Ndabila (kushoto)) akizungumza na wajane na wagane wakati wa hafla ya kukabidhi  msaada wa chakula (mchele) nguo na fedha iliyofanyika leo Desemba 26, 2022.

Mjumbe wa Serikali ya mtaa wa Mandela, Tabrisa Bushiri akitoa neno la shukurani.
Mke wa Askofu Ndabila, Janeth Ndabila  akitoa nguo katika hafla hiyo.
Mke wa Askofu Ndabila, Janeth Ndabila akitoa msaada wa nguo katika hafla hiyo.
Mjumbe wa Serikali ya Mtaa huo Juma Hassan akizungumza.
Wajane wakiwa kwenye hafla hiyo.
Hafla ikiendelea.
Mchele ukiwa kwenye mifuko tayari kwa kugaiwa walengwa.
 Nguo za aina mbalimbalizilizotolewa kwa walengwa.

Picha ya pamoja baada ya kutolewa kwa msaada huo.

Na Dotto Mwaibale, Dar es Salaam. 

KANISA la Abundant Blessing Church (ABC) lililopo Mtaa wa Mandela jijini Dar es Salaam limetoa msaada wa chakula, nguo za aina mbalimbali, viatu na fedha kwa ajili ya kuwasaidia Wagane na Wajane 40 wanaoishi kwenye mtaa huo..

Akizungumza  wakati wa kukabidhi msaada huo Askofu mkuu wa kanisa hilo hapa nchini, Flaston  Ndabila alisema wamekuwa wakiguswa na changamoto mbalimbali za Wajane na wagane na makundi mengine yanayoishi jirani na kanisa hilo na maeneo mengine ya jirani na kuwa  wameweka utaratibu kila mwaka kutoa msaada huo.

"Huu ni mwaka wetu wa sita tumekuwa tukifanya hivi  hasa kipindi hiki cha Sikukuu za mwishoni mwa mwaka za Krismas na mwaka mpya na leo tumetoa msaada huu ikiwa ni kuadhimisha siku ya kupeana zawadi baada ya krismas (Boxing day) alisema Ndabila.

Ndabila alisema kutoa msaada kwa makundi hayo ni kuchota baraka kutoka kwa Mungu kwani hata vitabu vya dini zote ya kikristo na kiislam vinaeleza hivyo.

Ndabila alisema nguo hizo zimetolewa na waumini wa kanisa hilo kwa ajili ya kusherehekea boxing day kwa makundi hayo.

 Baadhi ya wagane na wajane waliopata msaada huo waliushukuru uongozi wa kanisa hilo kwa msaada ambao wamekuwa wakiutoa kwako hasa Askofu wa kanisa hilo, Flaston Ndabila na mke wake Janeth Ndabila.

"Kwa kweli hatuna cha kueleza zaidi ya kutoa shukurani zetu na Mungu awape afya njema na maisha marefu" alisema. Khadija Hamisi.

Mjumbe wa Serikali ya mtaa huo, Juma Hassan alisema kanisa hilo limekuwa la mfano katika kusaidia jamii ya eneo hilo kwa mambo mbalimbali na hata wakati wa mafuriko limekuwa likijitoa kurekebisha miundombinu pamoja na kuwafariji wahanga.

"Kanisa la ABC hakika ni kanisa lenye uongozi thabiti limekuwa likishirikiana na Serikali kwa mambo mengi na hata kuwanunulia madaftari na vifaa wanafunzi ambao hawana uwezo" alisema Hassan.

Alisema Askofu wa kanisa hilo Flaston Ndabila kila inapofika mwishoni mwa mwaka amekuwa akiwakumbusha kwa ajili ya kutoa misaada hiyo japo ambalo linapendeza hata mbele za Mungu.

Friday, December 23, 2022

SHILINGI 67 MILIONI KUTEKELEZA MIRADI YA MAENDELEO JIMBO LA SINGIDA MASHARIKI

 Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki Miraji Mtaturu  akiongoza kikao cha kamati ya mfuko wa Jimbo kilichoketi jana Disemba 22, 2022 jimboni humo. Kushoto ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi, Ally Mwanga.

Na Dotto Mwaibale, Singida 

ZAIDI ya Sh.67 Milioni zimeelekezwa kuchagiza na kuchochea miradi mbalimbali ya maendeleo katika Jimbo la Singida Mashariki.

Akizungumza Disemba 22,2022 wakati akiongoza kikao cha kamati ya mfuko wa Jimbo, Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki Miraji Mtaturu alisema fedha hizo zinakwenda kutekeleza miradi mbalimbali kwenye jimbo hilo na akaomba zikatumike kukamilisha miradi yenye viwango na thamani halisi ya fedha hizo.

 Katika hatua nyingine   Taasisi ya Tanzania Youth  Elite Community (TYEC) kwa kuutambua  uzalendo  halisi wa nchi imemtunuku tuzo ya heshima mbunge huyo ikiwa ni kutambua juhudi zake katika kuchagiza maendeleo ya wananchi jimboni humo.

Katibu Mtendaji wa Taasisi hiyo Shigela Denis alisema wameamua kumtunuku tuzo hiyo kutokana na mchango wake mkubwa anaoufanya wa kuwaletea maendeleo wananchi wa jimbo hilo.

"Mbunge Mtaturu amekuwa ni chachu kubwa ya maendeleo katika jimbo la Singida Mashariki na kwa kipindi kifupi ambacho amekuwa katika jimbo hilo amefanya mambo makubwa na kwa kulitambua hilo kupitia taasisi yetu tumeamua kumtunuku tuzo hii ya heshima" alisema Shigela,

Akizungumza baada ya kutunukiwa tuzo hiyo aliishukuru taasisi kwa kutambua mchango wake na kueleza  tuzo hiyo ni ya Heshima kwa wananchi wote wa Wilaya ya Ikungi na si peke yake.

Katibu Mtendaji wa  Taasisi ya Tanzania Youth  Elite Community (TYEC)  Shigela  Denis akimkabidhi tuzo ya heshima (cheti) Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki Miraji Mtaturu ikiwa ni kutambua mchango wake mkubwa wa maendeleo katika jimbo hilo.


Picha ya pamoja baada ya kukabidhiwa tuzo hiyo.
Kikao cha kamati ya mfuko wa jimbo kikiendelea.
Mjumbe wa kamati ya mfuko wa jimbo hilo, Yahaya Njiku akichangia jambo kwenye kikao hicho. 

Thursday, December 22, 2022

MBUNGE SINGIDA MJINI ATOA MILIONI 5 KUCHANGIA UJENZI WA ZAHANATI

 Mbunge wa Jimbo la Singida Mjini Mwalimu Mussa Sima (katikati) akiwa katika picha na Wazee baada ya kufanya kikao na baraza la wazeewa Kata ya Unyianga katika ziara yake aliyoifanya juzi ya kutembelea na kukagua miradi ya maendeleo.

Na Dotto Mwaibale, Singida. 

MBUNGE wa Jimbo la Singida Mjini Mwalimu Mussa Sima ametoa Sh. Milioni 5 kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa Zahanati ya Unyianga iliyopo Manispaa ya Singida ambapo Serikali ilitoka Sh. 50 Milioni.

Ujenzi wa Zahanati hiyo umekwisha kamilika na tayari watumishi wawili wamekwisha fika ambao ni daktari na muuguzi.

Akizungumza wakati wa ziara yake aliyoifanya juzi Desemba 20, 2022 ya kukagua miradi ya maendeleo Sima alisema Serikali umefanywa kazi kubwa katika jimbo kwa kutoa Fedha nyingi.

Miradi aliyoitembelea na kuikagua ni ujenzi wa Shule ya Sekondari katika kata hiyo, ujenzi wa madarasa mawili shule ya Msingi ambapo alichangia Sh. 2 Milioni na kukagua ujenzi wa barabara za Kindai-Unyianga inayojengwa sambamba na madaraja na kunyanyua tuta barabara ya Unyianga Mwankoko.

Alisema barabara hiyo imekamilika baada ya  Serikali Kuu kutoa Sh.370 Milioni fedha ambazo zimechagiza kuchochomea kasi ya maendeleo katika jimbo hilo.

Katika hatua nyingine Mbunge Sima alipata fursa ya kuzungumza na baraza la wa wazee wa kata hiyo sanjari na kula nao chakula.

Aisha Sima alizungumza na makundi ya wauza kahawa na vikundi vya akina mama na kukiunga mkono kwa kukipa Sh   120, 000 na  kikundi cha wauza kahawa  Sh 70, 000 na kuwapongeza kwa umoja wao.

Katika ziara hiyo Mbunge Sima aliongozana na Diwani wa Kata ya Unyianga,  Geofrey  Mdama ambapo alitumia nafasi hiyokumpongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha nyingi kwa ajili ya kutekeleza miradi hiyo ya maendeleo.

Mbunge Sima akitoa mchango kuwaunga mkono wauzaji wa Kahawa wakati wa ziara hiyo.
Mbunge Sima akibadilishana mawazo na Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Unyianga wakati wa ziara hiyo. 

Tuesday, December 20, 2022

AIRTEL YAIUNGA MKONO BODI YA FILAMU TANZANIA KUFANIKISHA TAMASHA LA TUZO ZA FILAMU TANZANIA 2022, JOTI AWA KINARA


 Rais wa Shirikisho la Sanaa za Maonesho Tanzania Bi. Synthia Henjewele akimkabidhi Balozi wa Airtel Tanzania Lucas Mhuvile almaarufu Joti Tuzo Filamu Bora - Ucheshi (Best Comedy) kupitia Tuzo za Filamu Tanzania 2022 zilizofanyika Disemba 17, 2022 Ukumbi wa Mikutano wa  Kimataifa  wa AICC jijini Arusha.
...................................................
.
Na Mwandishi Wetu, Arusha.

KAMPUNI ya Airtel Tanzania inayotoa huduma za mawasiliano ya simu imekuwa sehemu ya kuunga mkono juhudi za Serikali katika kuinua Sekta ya Filamu naMichezo ya Kuigiza nchini ambapo ilikuwa moja ya Makampuni yaliyodhamini Tamasha la Tuzo za Filamu Tanzania linaloratibiwa na Serikali kupitia Taasisi yake ya Bodi ya Filamu Tanzania.

Kilele cha Tamasha la Tuzo za Filamu Tanzania 2022 kimefanyika Tarehe 17 Disemba, 2022 jijini Arusha katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano Arusha - AICC,ni Tamasha la pili kuratibiwa na Serikali kupitia Bodi ya Filamu, ambapo limetoa jumla ya washindi wa Tuzo 32 kutoka katika Filamu 59 zilizofanikiwa kuingia kwenye kinyang’anyiro. Aidha, Tamasha la kwanza lilifanyika mwaka 2021 jijini Mbeya.

Akizungumza katika usiku wa kilele hicho Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Mohamed Mchengerwa ambaye pia alikuwa mgeni rasmi alisisitiza kuwa,dhamira ya Serikali ni kuendelea kuwekeza katika kuwasaidia Wasanii ili waweze kufanya vizuri, ambapo tayari Serikali imeanzisha Mfuko wa Utamaduni na Sanaa ambao utaanza kutoa mikopo kwa Wasanii kuanzia jumatano ya Disemba 21, 2022.

“Sekta ya Filamu inakua, na inaendelea kutoa ajira kwa vijana wengi pamoja na kuchangia katika Pato la Taifa, hivyo sisi kama Serikali tutaendelea kuweka nguvukatika Sekta hiyo" amesema Mhe. Mchengerwa.

Kwa upande wake Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania Dkt. Kiagho Kilonzo alisema nia ya Serikali ya kuanzisha Programu hii ya kutunuku wadau wake Tuzo ni:

 “kutambua mchango wa wanatasnia ya Filamu,b. kutambua vipaji vilivyojificha vya wanatasnia ya Filamu,c. kuongeza hamasa kwa wanatasnia ya kuzalisha kazi nyingi zaidi za Filamu,d. kuongeza hamasa kwa wanatasnia ya Filamu kuzalisha kazi bora za Filamuna hatimaye kuwa na ushindani mkubwa ndani na nje ya nchi, nae. kusisimua fursa za uwekezaji katika Sekta ya Filamu nchini”.

Aidha, kupitia zoezi hili zima la Tamasha la Tuzo hapa nchini, Serikali itapata Taswira itakayoweza kusaidia kuandaa program maalumu za kuwajengea uwezo watendaji wetu wa filamu kulingana na mahitaji yao halisi.

Kampuni ya Airtel Tanzania ilikuwa moja ya Makampuni yaliyodhamini Tamasha laTuzo za Filamu 2022 na iliwakilishwa na Meneja wa Kanda ya Kaskazini Bi. MonicaErnest ambapo alipata nafasi ya kukabidhi Tuzo ya Filamu bora - Mapambo Atharikwa mshindi wa kipengele hicho Bw. Jafari Athumani kupitia Filamu ya Mateka.

Aidha, Meneja huyo alisema kuwa Kampuni ya Airtel Tanzania imekuwa mstari wa mbele katika kusaidia Sekta za Sanaa hususani Filamu, ambapo imeanzisha Televisheni Mtandao (Airtel Tv) yenye lengo la kusaidia Wasanii wa Filamu nchini kuuza kazi zao kupitia mtandao huo, ambapo wasanii hao wanapata fedha kutokana na wingi wa watazamaji ndani na nje ya nchini hivyo kuongeza pato la Wasanii mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla kupitia kodi.

WACHAKATAJI WA MAZAO YA UVUVI MKOANI KIGOMA WAPIGWA MSASA

Mkurugenzi Msaidizi anayesimamia masuala la Udhibiti Ubora wa Mazao ya Uvuvi na Masoko, kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Bw. Steven Lukanga akizungumza katika mafunzo ya kuwajengea uwezo wachakataji wa mazao ya uvuvi Ziwa Tanganyika mkoani Kigoma (kulia ) ni Afisa Mtaalam Mnyororo wa  Thamani wa Uvuvi na Ufugaji Viumbe Maji  Hashim Muumin.

Na Devotha Songorwa, Kigoma

WACHAKATAJI wa mazao ya uvuvi nchini wametakiwa kutumia fursa ya teknolojia katika shughuli zao ili kuboresha mnyororo wa thamani wa mazao ya uvuvi na kukabiliana na upotevu wa mazao hayo katika Ziwa Tanganyika.

Hayo yamesemwa na Afisa Mtaalam Mnyororo wa  Thamani wa Uvuvi na Ufugaji Viumbe Maji  Hashim Muumin  wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wachakataji, wavuvi na  wafanyabiashara yaliyoandaliwa na Shirika la Chakula na Kilimo Duniani (FAO) kupitia miradi yake ya  FISH4ACP  na Flexible Multi-partner Mechanism (FMM) mafunzo  ambayo yamefanyika mkoani Kigoma.

Afisa huyo alisema mradi wa FISH4ACP unatekelezwa katika nchi 12 za Africa, Caribbean na Pacific ambapo nchini Tanzania unafanyika katika Mikoa ya Katavi, Rukwa na Kigoma ukilenga kukabiliana na changamoto  za upotevu wa mazao ya samaki kabla na baada ya shughuli za uvuvi, wakati wa uchakataji wa samaki na wakati wa kusafirishwa kwenda kwenye masoko ya ndani na nje ya nchi.

“Mafunzo haya yamefanyika kwa njia ya filamu zilizonakiliwa kutoka Kenya, Uganda na Ghana lengo ni kuwawezesha wachakataji kujifunza njia bora za kuchakata mazao yao kama tulivyoona  kwa wenzetu wanatumia majiko banifu, chanja rafiki na salama za kuanikia dagaa,”alisema.

Pia ameongeza kuwa kupitia miradi hiyo wanatarajia kujenga miundo mbinu  ya kuchakatia dagaa na samaki  itakayoendana na mabadiliko ya tabia Nchi ambapo kwa sasa hatua zilizochukuliwa ni ufuatiliaji wa maeneo sahihi ya kuchakatia.

“Kama mradi tutatengeneza majiko ya kubanikia samaki tupate bidhaa nzuri kutoka Ziwa Tanganyika na tutaendelea na ufuatiliaji kuona kama mafunzo haya yanatafanya kazi kama tulivyokusudia na yatasaidia changamoto iliyopo sasa ya mabadiliko ya  tabianchi ,” alieleza.

Kwa upande wake Mkurugenzi Msaidizi anayesimamia masuala la Udhibiti Ubora wa Mazao ya Uvuvi na Masoko, kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Bw. Steven Lukanga alibainsiha kuwa sekta ya uvuvi inachangia karibu asilimia 1.8 ya pato la Taifa wakati ulaji ukichangia asilimi 30 ya virutubishi vitokanavyo na wanyama.

“Ulaji wetu unaonekana tunakula wastani wa kilo 8. 5 badala ya kilo 20.5 kwa mwaka hivyo mafunzo haya yamekuja wakati muafaka yatasaidia kuboresha shughuli zetu tunazofanya hasa unapovua samaki wako au dagaa uhakikishe unawahifadhi sehemu salama na hata ukaushaji wetu uwe wenye manufaa kimasoko,” alifafanua.

Naye Afisa Uvuvi anayesimamia Wilaya ya Uvinza Bw. Venance Msongambele alisema elimu hiyo itawasaidia wadau wa uvuvi na wachakataji kuepuka kufanya kazi kwa mazoea,  na badala yake watakausha  samaki kwa kutumia mkaa  hatua inayoongeza thamani ya mazao hayo na kuvutia wateja.

“Kuna maboresho ambayo yakifanyika  yatatusaidia sana kama kupata barafu kuhifadhi samaki na dagaa, majiko ya mkaa  kwa sababu kuni siyo salama kwa afya kutokana na moshi  na kupitia mafunzo haya tumejifunza kufanya uchakataji kwa kuzingatia uhifadhi wa mazingira,”alieleza afisa huyo.

Akitoa shukrani zake Mchakataji kutoka Mwalo wa Katonga mkoani Kigoma Selestina  Silvester ameipongeza FAO kwa kuandaa semina hiyo kwani itawasaidia katika uhifadhi wa rasilimali za Ziwa Tanganyika kwa manufaa yao na Nchi kwa ujumla.

“Tunaishukuru sana FAO kwa kutoa  na elimu hii  inatusogeza kutoka hapa tulipo hadi sehemu nyingine  kwa sasa uchakataji tunafanya kienyeji sasa unakuta samaki au dagaa wanaharibika haraka kabla ya kufika sokoni na wanapungua ubora,”alisema Selestina. Afisa Mtaalam Mnyororo wa  Thamani wa Uvuvi na Ufugaji Viumbe Maji  Hashim Muumin.

Aidha Mwenyekiti wa Vyama vya Wavuvi Mkoa wa Kigoma Bwa. Francis John aliwahimiza wadau hao kutumia ujio wa mradi huo kama fursa muhimu kwao kuongeza thamani ya bidhaa zao ili kuendana na hali ya soko la sasa.

Baadhi ya wadau wa sekta ya uvuvi wakifuatilia mafunzo hayo kutoka kwa wawezeshaji (hawapo pichani).

Picha ya pamoja baada ya mafunzo hayo.

Afisa Mtaalam Mnyororo wa  Thamani wa Uvuvi na Ufugaji Viumbe Maji  Hashim Muumin akifafanua jambo wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wachakataji wa mazao ya uvuvi mkoani Kigoma.

Monday, December 19, 2022

MBUNGE SINGIDA MJINI MUSSA SIMA ADHAMINI NA KUZINDUA LIGI YA MINGA CUP

Mbunge  wa Jimbo la Singida Mjini Mussa Sima akizungumza wakati wa uzinduzi wa mashindano ya ligi ya mpira wa miguu ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Kata ya Minga yajulikanayo  Minga Cup katika hafla iliyofanyika jana Desemba 19, 2022 Uwanja wa Shule ya Msingi Minga Manispaaya Singida..
Mbunge Sima akimtambulisha Diwani wa Kata ya Mwankoko, Emmanuel Emadaki ambaye alikuwa ameongozana naye kwenye uzinduzi wa mashindano hayo.
Mwenyekiti wa UVCCM Kata ya Minga, Masanja Christopher akizungumza wakati wa uzinduzi wa mashindano hayo.
Diwani wa Kata ya Minga, Ibrahim Mrua akizungumza wakati wa uzinduzi huo.
Mbunge wa Singida Mjini Mussa Sima akimkabidhi mpira Mwenyekiti wa UVCCM Kata ya Minga, Masanja Christopher.
Mbunge wa Singida Mjini, Mussa Sima (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wachezaji na washiriki wa uzinduzi wa mashindano hayo. 

Na Dotto Mwaibale, Singida. 

MBUNGE wa Jimbo la Singida Mjini Mussa Sima amedhamini na kuzindua mashindano ya ligi ya mpira wa miguu ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) katika Kata ya Minga yajulikanayo  Minga Cup.

Mashindano hayo yaliyozinduliwa jana katika Uwanja wa Shule ya Msingi Minga yamelenga kuwaweka pamoja vijana wa kata hiyo sanjari na kuimarisha afya zao

Kwenye uzinduzi huo Mbunge Sima alitoa mpira kwa ajili ya mashindano hayo  ambayo fainali yake inatarajiwa kuwa Desemba 31, 2022.

Akizungumza na washiriki wa mashindano hayo Sima alisema michezo ni afya,ajira,upendo,mshikamano na kuwa  inaleta urafiki,umoja,ujamaa,ushirikiano katika masuala mbali mbali.

Aidha Sima aliahidi kuendelea kuwaunga mkono vijana katika jimbo hilo katika masuala mbalimbali yenye tija ikiwemo michezo.

Katika uzinduzi huo Mbunge Mussa Sima aliongozana na Diwani wa Kata ya Mwankoko, Emmanuel Emadaki.