Sunday, December 6, 2020

WANACHUO WENYE ULEMAVU SINGIDA WAKOSA UZIO

Mgeni rasmi wa Mahafali ya 42 ya Chuo cha Ufundi na Marekebisho kwa Watu wenye Ulemavu Sabasaba VTC Singida, ambaye pia ni Kaimu Meneja Mradi wa Kampuni ya Uchimbaji Madini ya Shanta, Elisante Kanuya, akihutubia mahafali hayo jana.
Mkuu wa Chuo cha Ufundi na Marekebisho kwa Watu wenye Ulemavu Sabasaba VTC Singida, Fatma Malenga akizungumza wakati wa sherehe za mahafali hayo.
Mwanachuo aliyebobea kwenye fani ya maandishi ya Nukta Nundu, Malingira Mathias akionyesha umahiri wake kwa kuandika jina la mgeni rasmi kupitia mashine ya Braille.
Mwanachuo wa fani ya umeme majumbani, Masome Stephano, akionyesha namna alivyokidhi vigezo vya kuwa fundi wa taaluma hiyo mbele ya wageni waliofika chuoni hapo jana.
Wahitimu wakiingia kwenye viwanja vya chuo hicho kabla ya kuanza sherehe za mahafali hayo.
Wahitimu wa mahafali hayo.
Wahitimu wa mahafali hayo wakifurahia.
Wahitimu wakifuatilia matukio mbalimbali yanayoendelea.
Wageni waalikwa wakiwa kwenye picha ya pamoja .
Mwanachuo Zanura Mohamed akiwafafanulia wahitimu wenzake kupitia lugha ya alama, hususani wale wenye ulemavu wa kusikia hatua kwa hatua kuhusiana na matukio yote yaliyokuwa yakiendelea kwenye sherehe hizo.
Mhitimu wa kozi fupi fani ya mapambo chuoni hapo, Edna Alex, akipokea cheti cha kuhitimu mafunzo.
Mmoja wa wahitimu akipokea cheti cha kuhitimu mafunzo.
Afisa Uhusiano wa Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka mkoa wa Singida (SUWASA), Grace Lolo akilishwa kipande cha keki na mmoja wa wahitimu chuoni hapo kama shukrani kwa mamlaka hiyo kwa kuchangia shilingi laki moja kwa ajili ya shughuli ndogondogo zilizofanikisha kufanyika kwa mahafali hayo.
Katibu wa Wazazi Chama Cha Mapinduzi  mkoa wa Singida, Ibrahim Mpwapwa, akilishwa kipande cha keki na mhitimu Edna Alex, kama shukrani kwa mchango wake kukamilisha kufanyika kwa mahafali hayo.
Meneja wa Karakana ya shirika la SEMA lililopo mkoani Singida, Lameck Muyanzi, akilishwa keki na muhitimu Zanura Mohamed ambaye mafunzo yake chuoni hapo yanafadhiliwa na shirika hilo kupitia mradi ujulikanao kama YES.
Wanachuo wengine wakifuatilia sherehe za mahafali hayo.
Sherehe zikiendelea.
Sherehe zikiendelea.
Sherehe zikiendelea.
Mafunzo kwa vitendo katika mahafali hayo.
 



Na Godwin Myovela, Singida


CHUO cha Ufundi na Marekebisho kwa Watu wenye Ulemavu Sabasaba VTC, mkoani hapa, kipo hatarini kiusalama kutokana na kukabiliwa na tatizo la kukosa uzio, hali inayoweza kusababisha wanafunzi wake ambao wengi wao ni wenye matatizo ya mtindio wa ubongo, na aina nyingine ya ulemavu kuwa katika hatari ya kupata majanga mbalimbali.

Endapo waangalizi watajisahau, au serikali kuendelea kufumbia macho changamoto hiyo, basi; kuna hatari ya wanachuo hao, hususani wale wenye mtindio wa ubongo na albino kuwa katika hatari ya kupotea, kudhurika na watu wenye nia mbaya au kupata ajali-kutokana na chuo hicho kuwa jirani na barabara ambayo hata hivyo haijawekewa matuta.

Akizungumza kwenye sherehe za  mahafali ya 42 jana, Mkuu wa chuo hicho, Fatma Malenga, aliwaomba wadau na watu wengine wenye mapenzi mema kujitokeza kusaidia kutatua changamoto zilizopo kwa muktadha chanya wa usalama wa watoto hao, wakati juhudi nyingine za serikali katika kutatua changamoto hiyo zikiendelea.

“Pamoja na mafanikio tuliyonayo, uongozi wa chuo unakabiliwa na changamoto kubwa ya ulinzi na usalama. Eneo la chuo ni kubwa lakini halina uzio,” alisema Malenga.

Changamoto nyingine zinazokikabili chuo hicho ni pamoja na upungufu wa madarasa na karakana ambazo ni kitovu cha mafunzo ya nadharia na vitendo-kwa mantiki ya kustawisha ujuzi na stadi zao katika uhalisia wa kukabiliana na teknolojia za kisasa kwenye kujiajiri au kuajiriwa, punde wanapohitimu mafunzo yao.

Kwa mujibu wa Malenga, kwa mwaka huu pekee chuo hicho kimepokea jumla ya wanachuo 228, kati yao 125 ni wanafunzi wa kozi fupi, na 103 kozi ndefu, huku idadi ya wenye ulemavu wanawake na wanaume ikifikia 60.

Mmoja wa wahitimu wa fani ya mapambo chuoni hapo, Edna Alex, aliomba pia serikali na wadau waangalie uwezekano wa kujenga haraka ukumbi kwa ajili ya sherehe na mikutano mbalimbali ya ndani ya chuo, kutokana na vijana hao mchanganyiko kukosa maeneo rasmi ya kukusanyikia na kupeana mrejesho wa mambo yao kadha wa kadha.

Awali, akitoa nasaha kwa wahitimu, mgeni rasmi wa mahafali hayo, ambaye pia ni Kaimu Meneja wa Mradi wa Kampuni ya Uchimbaji Madini ya Shanta, yenye matawi yake Singida na Songwe nchini, Elisante Kanuya, aliitaka jamii kuunga mkono kwa kununua au kusaidia upatikanaji wa masoko kwa bidhaa zote za kazi za mikono zinazozalishwa chuoni hapo.

Kanuya alisema Kampuni ya Shanta kwa tawi la Singida, ambayo kwa sasa inajulikana kama ‘Singida Gold Mine inatarajia kuanza rasmi uzalishaji wake ifikapo 2022, huku akiwataka wahitimu wa chuo hicho kuhakikisha muda ukifika wanachangamkia fursa za ajira zitakazojitokeza ili kuleta ustawi wa vipato, lakini pia kuwa sehemu ya kulisaidia taifa na maono ya Rais John Magufuli katika kufikia uchumi wa juu.

“Mafunzo haya mliyopata yakawasaidie kujenga taifa, mkawe chanya na alama ya maendeleo. Tutafurahi sana kuwaona mkiwa wengi ndani ya Kampuni ya Shanta pale tutakapoanza kuzalisha ajira za kutosha,” alisema Kanuya.

Chuo hicho kinachotoa mafunzo ya ufundi na marekebisho kwa watu wenye ulemavu Singida, ambacho imeelezwa huko nyuma kilijulikana kama ‘Chuo cha Wanawake Wasioona’  kilianzishwa mwaka 1977 kwa ushirikiano wa serikali ya Tanzania na Sweden, lengo likiwa ni kutoa huduma za marekebisho sanjari na kuwawezesha watu wenye ulemavu kupata ajira na kujitegemea kiuchumi.

Hata hivyo kwa sasa kipo chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu, na kinaendelea mpaka sasa kutoa mafunzo ya ufundi stadi kwa vijana wenye ulemavu wa aina zote kwa gharama ya serikali. 

“Wanafunzi wanaopokelewa ni wenye umri wa miaka 15 mpaka 35 wakiwemo watumishi wa umma ambao wamepata ulemavu…huku chuo kwa sasa kikiendelea kupokea wanafunzi wenye ulemavu wa ngozi, viziwi, wenye ulemavu wa viungo, wasioona na wenye tatizo la mtindio wa ubongo kwa jinsia zote,” alisema Malenga na kuongeza:

“Huduma za kimafunzo zinazotolewa chuoni hapa ni pamoja na mafunzo ya fani za ufundi wa umeme majumbani, useremala, ushonaji, maandishi ya nukta nundu, kilimo, mapishi na maarifa ya nyumbani, afya ya uzazi na stadi za kazi, ‘technical drawing’, sayansi ya kompyuta, huduma ya ushauri wa aina ya ajira na ushauri nasaha kwa wenye ulemavu hususani walioathiriwa na unyanyapaa ndani ya jamii.”

Friday, December 4, 2020

ONGEZEKO LA VIPATO KWA WATU WA MJINI VIMECHANGIA MATUMIZI YA MAZAO YA MIFUGO NA UVUVI

Mkurugenzi wa wa Sera na Mipango wa Wizara hiyo,  Amosy Zephania   wakati wa ufunguzi wa Kongamano la 43 la uzalishaji na uendelezaji wa mifugo na mkutano wa 44 wa mwaka wa chama cha Wataalamu wa uzalishaji na uendelezaji wa mifugo Tanzania (TSAP) kilichofanyika Jijini Dodoma.

Mwenyekiti wa wa chama cha wataalamu wa uzalishaji na uendelezaji wa Mifugo Tanzania (TSAP) Dkt. Daniel Komwihangilo akitoa salamu za chama hicho wakati wa ufunguzi wa kongamano hilo.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma,   Maduka Kessy akitoa salamu za mkoa mbele za wajumbe wa chama hicho.
Mratibu wa dawati la sekta binafsi Wizara ya Mifugo na Uvuvi  Steven Michael akichangia kwenye mkutano huo.
Picha ya pamoja ya mgeni rasmi na wananchama wa TSAP mara baada ya ufunguzi wa kongamano hilo.
 




Na Calvin  Gwabara, Morogoro.


Imebainishwa kuwa kadri watu wanaokaa mijini vipato vyao vinavyozidi kukua na kuongezeka ndivyo matumizi na mahitaji ya mazao ya mifugo na uvuvi yanavyoongezaka hivyo uzalishaji wa mifugo na samaki lazima uboreshwe ili kukidhi mahitaji hayo.

Hayo yamebainishwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Mifugo Prof. Elisante Ole Gabriel kwa niaba yake na Mkurugenzi wa wa sera na mipango wa Wizara hiyo Amosy Zephania   wakati wa ufunguzi wa Kongamano la 43 la uzalishaji na uendelezaji wa mifugo na mkutano wa 44 wa mwaka wa chama cha Wataalamu wa uzalishaji na uendelezaji wa mifugo Tanzania (TSAP)kilichofanyika Jijini Dodoma.

Alisema kuwa Mahitaji ya lishe na protini inayotokana na Mifugo yanatarajiwa kuongezeka kwa kiasi kikubwa katika miaka 20 ijayo kutokana na ongezeko la watu,kukua kwa miji na kuongezeka kwa kipato cha watu hivyo ni wakati muafaka sasa kufanya mapinduzi makubwa katika uzalishaji na minyororo ya thamani ya mifugo na samaki ili kukidhi mahitaji ya uchumi wa viwanda pia.

" Hapa nchini kwetu uzalishaji wa mazao ya Mifugo haukui kwa viwango vinavyotakiwa kama yalivyo mahitaji ya walaji,hii inaleta umuhimu wa kufanya mabadiliko katika mifumo yetu na kuongeza ufanisi na tija ya uzalishaji kwa kutumia sayansi na teknolojia za kisasa" Alisema Profesa. Elisante.

Katibu Mkuu huyo alisema mifumo ya uzalishajiwa Mifugo na Uvuvi nchini imeegemea zaidi kwenye uzalishaji kwa njia ya mifumo ya asili ambapo Wazalishaji wengi ni Wafugaji na Wavuvi wadogowadogo na mifumo mingi iliyopo bado ni ya asili yenye viwango vidogo na hairidhishi.

Alieleza kuwa kuna haja ya kuongeza upatikanaji wa malighafi zinazotakiwa katika viwanda vya kusindika mazao ya Mifugo na Uvuvi na kuhimiza  Wafugaji na wazalishaji  kuwekeza katika teknolojia na vitendea kazi sahihi vitakavyoongeza uzalishaji mashambani na kuwezesha kufikia masoko kwa ufanisi zaidi.

"Ninayasema haya yote nikiwa na nia ya dhati kwamba sekta ya Mifugo na Uvuvi bado zina changamoto nyingi na nyinyi Wataalamu na wadau lazima muone ulazima wa kuzikabili na kuzitafutia suluhu na changamoto nyingine nizigusie tuu ambazo ni uharibifu wa ardhi kutokana na mmomonyoko pamoja na mahitaji ya maji safi ya kunywa kwaajili ya mifugo sambamba na mahitaji ya malisho bora na ya kutosha" Alisisitiza Profesa. Elisante.

Akizungumza kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi kufungua Kongamano hilo Mwenyekiti wa wa chama cha wataalamu wa uzalishaji na uendelezaji wa Mifugo Tanzania (TSAP) kt. Daniel Komwihangilo lisema kuwa chama chao kinaona ni wakati muafaka sasa wa Serikali kutunga sheria ambayo itadumisha udhibiti na usimamizi wa mazoezi halali ya sayansi ya wanyama na kazi ya uzalishaji kama ambavyo ilivyo kwa vyama vingine kama Wahandisi,Wanasheria na wengine wengi.

Alifafanua kuwa kupitia sheria hiyo wataalamu wa sayansi za wanyama na uzalishaji watakuwa na Mdhibiti/Msajili ambaye atahakikisha wataalamu hao wanafuata na kutii sheria na hivyo kulinda maslahi ya Mfugo,Wafugaji na wadau wengine.

Alifafanua kuwa Mda kuu ya mkutano huo wa kisayansi wa 43 ni kuinua viwango vya minyororo ya thamani ya Mifugo na Uvuvi kwa mafanikio endelevu kijamii na kiuchumi lakini kuna mada nyingine ndogo nyingi ambazo zimejikita kwenye maeneo mahususi ya ukuaji wa teknolojia na matumizi ya yake katika kuboresha wa Mifugo na viumbe maji pamoja na matumizi  yake katika uzalishaji bora,ufugaji na sera.

"Ni nafasi sasa kwa wizara husika inayoshughulikia maendeleo ya Mifugo nchini kuchukua hatua hii na sisi kama TSAP tupo tayari kutoa ushrikiano wowote utakaohitajika katika jitihada hizi" Alisema Dkt. Komwihangilo.

Dkt. Komwihangilo amesema TSAP wameomba eneo lenye ukubwa wa mita za mraba 7680 kwenye jiji la Dodoma ambalo wanaamini wataliendeleza kwaajili ya kusaidias kutoa huduma za ushauri kwa Wafugaji,Wanafunzi na wadau wengine kirahisi hivyo wanahitaji kiasi cha shilingi milioni 36,827,674 kulinunua.

Wednesday, December 2, 2020

NDAHANI APONGEZA UFANISI VETA SINGIDA...AWAFUNDA WAHITIMU

Kaimu Afisa Vijana Mkoa wa Singida ambaye ni mgeni rasmi wa Mahafali ya 31 VETA-Singida, Frederick Ndahani akihutubia sherehe za mahafali hayo juzi.


Wahitimu wakijiandaa kuingia ukumbini.

Wazazi na baadhi ya walimu wakishiriki sherehe hizo.
Wazazi na baadhi ya walimu wakishiriki sherehe hizo.
Wanachuo wa VETA Singida-wakifuatilia matukio ya sherehe hizo.

Baadhi ya wahitimu wakiwa kwenye picha ya pamoja.

Sherehe zikiendelea ndani ya ukumbi.


Baadhi ya wahitimu wakiwa kwenye picha ya pamoja.

Mkuu wa Chuo cha Veta-Singida, Paul Batoleki akimpongeza mmoja wa wahitimu.

Ndahani akikabidhi vyeti kwa wahitimu.

Mgeni rasmi akiwa kwenye karakana ya Ufundi Bomba.

Mratibu wa Chama cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Singida (Singida Press), Domician Mwalusito (kulia) na Katibu wa chama hicho Revocatus Gervas wakiwa na mmoja wa wahitimu kwenye mahafali hayo.



Na Godwin Myovela, Singida


KAIMU Afisa Vijana mkoani hapa Frederick Ndahani amepongeza umahiri wa mafunzo na mifumo ya kiteknolojia inayotumika kutoa mafunzo ya nadharia na vitendo kwa vyuo vya VETA nchini, huku akiwataka wahitimu wake kutumia stadi za mafunzo hayo katika kulifikisha Taifa kwenye uchumi wa juu.

Ndahani alitoa pongezi hizo jana wakati akihutubia Sherehe za Mahafali ya 31 ya kuhitimu Mafunzo ya Ufundi Stadi VETA Singida.

"Tafsiri ya kuhitimu kwenu leo maana yake ni kuongeza tija kwa taifa letu na kuzidi kutatua changamoto ya upungufu wa ajira hususani kwa vijana," alisema.

Alisema ili kuikwamua nchi katika sekta mbalimbali serikali imejiwekea mikakati kadhaa ya utekelezaji, ikiwemo kuhuisha uwiano wa viwango vya mafunzo vyenye ujuzi wa juu yaani (Engineers), ujuzi wa kati (Technicians) na mafundi wa kazi za mikono (Artisans) kwa uwiano wa 1:5:25.

"Nawasihi tumieni ujuzi na umahiri mlioupata kwenye kujiajiri ili kujikwamua na wimbi la umasikini. Funguo ya mafanikio kwanza ni kuwa na ujuzi na maarifa, pili ni tabia na tatu ni vitendo," alisisitiza Ndahani.

Sanjari na kupongeza juhudi za serikali kupitia VETA Singida- kwa kuchagiza maendeleo ya vijana kiuchumi, Ndahani alitoa wito kwa wakurugenzi kuwatumia wahitimu wa vyuo hivyo na vijana wengine katika ujenzi wa miradi inayotumia 'Force Account'.

Alisema mfumo huo ulianzishwa na kutolewa maelekezo na Rais John Magufuli kwa maksudi, lengo likiwa ni kuwasaidia mafundi waliopo mitaani kupata ajira kupitia miradi hiyo.

Imeelezwa kwamba mfumo wa makandarasi umekuwa ukiwaumiza mafundi kwa kuwakosesha fursa mbalimbali hususani vijana wa kundi la kazi za mikono, huku baadhi ya Mabaraza ya Halmashauri na Wakurugenzi wakishindwa kusimamia ipasavyo.

"Niwasihi sana wakurugenzi kuwatumia sana vijana wa taifa hili wakiwemo hawa wanaopita kwenye mikono ya VETA katika ujenzi wa miradi hii ambayo kwa sasa ipo kila kona ya nchi" alisema Mgeni rasmi wa mahafali hayo Ndahani, ambaye pia ni Kaimu Afisa Vijana Mkoa wa Singida.

Kwa upande wake, mwenyeji wa mahafali hayo, Mkuu wa Chuo cha Veta-Singida, Paul Batoleki, alisema kupitia mahafali hayo, jumla ya wanachuo 156 wamehitimu fani mbalimbali kwa Ngazi ya Pili na Tatu.

Alizitaja fani hizo kuwa ni pamoja na Mifugo, Ufundi Magari, Uchomeleaji, Useremala, Ujenzi, Ushonaji, Umeme, na Ufundi Bomba, huku pia kukiwa na fani nyingine ya Uhazili na Kompyuta inayofundishwa chuoni hapo ambayo hata hivyo haikuwa na muhitimu kwenye mahafali hayo.

Batoleki alipongeza serikali kupitia Mamlaka hiyo ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi nchini kwa kutenga jumla ya shilingi milioni 340 Kwa ajili ya ujenzi wa madarasa na maabara chuoni hapo kwa fani ya ufugaji wa wanyama.

Awali, kupitia risala yao, wahitimu hao Kwa kuzingatia ongezeko la tija chuoni hapo wameiomba serikali kutatua uhaba uliopo wa baadhi ya vitabu vya masomo ya fani.

Changamoto nyingine ni mamlaka ziangalie uwezekano wa kuwagharamia wanafunzi wawapo kwenye mafunzo kwa vitendo, hasa kwenye maeneo ya viwanda ambako wengi hujikuta wakifanya 'fields' zao katika mazingira magumu.

"Tunaomba pia tuongezewe walimu wa masomo ya muambata mfano 'LifeSkills' lakini kubwa serikali iangalie uwezekano wa kutuongezea vifaa kulingana na teknolojia za kisasa ili kuongeza tija na ufanisi,"  alisema Rais Mstaafu wa Chuo hicho, Elisha Ezekiel.

Mkoa wa Singida una jumla ya viwanda 1,805 ambapo kati yake kiwanda kikubwa ni 1, kati 10, vidogo 309 na vidogo sana 1,485 hatua ambayo imeendelea kupanua wigo wa fursa za ajira hususani kwa makundi ya vijana na wanawake kulingana na fani mbalimbali walizonazo.


PINDA:KILIMO PEKEE NDICHO KITAONDOA UMASIKINI TANZANIA.

Katibu wa Chama cha Wachumi Kilimo Tanzania (AGREST) Dkt. Betty Waized akitoa salamu za Chama hicho na malengo ya mkutano huo kabla ya kumkaribisha Mgeni rasmi kwaajili ya ufunguzi. 
Waziri Mkuu Mstaafu wa Tanzania Mizengo Pinda akitoa nasaha zake mbele ya Wataalamu hao wa Uchumi Kilimo wakati akifungua rasmi mkutano huo wa 12 wa Kisayansi wa  Chama hicho mjini Dodoma.
Profesa. Aida Isinika akimkabidhi Pinda zawadi maalumu iliyotolewa na chama hicho kama kumbukumbu.
Mkutano ukiendelea.
Mkutano ukiendelea.
Mkutano ukiendelea.
Wanachama wa AGREST na Mgeni rasmi Mizengo Pinda mara baada ya ufunguzi wa mkutano huo wa 12 wa kisayansi.

Washiriki wa mkutano wakifuatilia hotuba za ufunguzi.
Washiriki wa mkutano wakifuatilia hotuba za ufunguzi. 


Na Calvin Gwabara, Dodoma


Imeelezwa kuwa Tanzania haitaweza kuondoa umasikini wala kupiga kasi ya Kim aendelee kwa Wananchi wake endapo swala la Kilimo Bora na cha kisasa halitapewa kipaumbele na Serikali, Watafiti na wadau wengine wa kilimo.

Hayo yamesemwa na Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mizengo Pinda wakati akifungua Kongamano la Kisayansi la Chama cha Wachumi Kilimo Tanzania (AGREST) lenye Mada kuu isemayo “Kuondoa vizuizi katika biashara ili kushanirisha biashara ya mazao ya Kilimo na mifumo ya chakula baina ya nchi za Afrika”lililofanyika mkoani Dodoma.

Pinda alisema pamoja na mabadiliko yanayoendelea katika shughuli za kiuchumi za watanzania katika maeneo ya vijijini zaidi ya asilimia 60 ya wananchi wanategemea kilimo lakini ni ukweli kwamba  wanaotegemea kilimo bado ni masikini kwa kiasi kikubwa wanategemea mazao ya chakula kama chanzo muhimu cha kipato cha kaya.

“ Juhudi za nchi  yetu za kuendeleza viwanda kwa kiasi kikubwa zinategemea uzalishaji na biashara ya mazao ya kilimo na hasa mazao ya chakula hivyo mada kuu ya kongamano hili ni muhimu sana katika ustawi wa Wananchi wengi ambao wanategemea moja kwa moja Kilimo cha mazao hayo au wale wanaofanya shughuli katika mnyororo wa thamani wa mazao hayo”  alisisitiza Pinda.

Alisema kuwa taarifa zilizopo zinaonyesha kuwa biashara ya mazao ya kilimo baina ya nchi za Afrika kwa sasa ni chini ya asilimia 20 huku ikikadiriwa kuwa tunakosa mapato Dola bilioni 30 kwa Mwaka kwa kutoboresha mazingira ya Biashara yetu ya Kilimo baina yetu wakati maeneo mengine nje ya Vara la Afrika yakifanya vizuri.

Pinda aliongeza kuwa kwa muongo mmoja na nusu Tanzania imeweza kupanda kutoka nafasi ya 10 Mwaka 2007 hadi kufikia nafasi ya 7 kama muuzaji mkubwa wa mazao ya kilimo ndani ya Afrika na kwamba muelekeo huo ni mzuri ingawa kuna mengi ya kufanya hasa ukilinganisha na uwezo na rasilimali zilizopo nchini.

Hata hivyo waziri mkuu huyo mstaafu alibainisha kuwa tafiti zinaonyesha kuwa

vikwazo visivyo kodi vinakwamisha zaidi biashara kuliko vikwazo vya kikosi na kwamba taarifa zilizopo zinaonyesha kuwa vikwazo visivyo kodi ni tatizo kubwa San katika kufanya biashara baina ya nchi za Afrika kuliko nchi zilizo nje ya Afrika.

“ Ni imani yangu kuwa katika kongamano hili mtajadili namna bora ya kutoka katika mzunguko au mkwamo huu” alisema Pinda.

Hata hivyo  Pinda alisema kwakuwa kilimo bodo kinaajiri watu wengi kuimarika kwa bishara ya mazao ya Kilimo kutaimarisha ajira za watu wengi na kufanya Kilimo kiwe ni ajira yenye kuvutia hasa vijana kwani benki ya dunia inakadiria hadi kufikia mwaka 2022 kutakuwa na watu bilioni 1.6 wanaohitaji ajira na Afrika pekee ni vijana milioni 25 wanaohitaji ajira kila mwaka.


“ Mimi binafsi ni muumuni wa kuwa maendeleo ya jamii ya jamii yoyote yanategemea sana matumizi ya taarifa za kutafiti ambazo zitasaidia wafanya maamuzi kuchukua Mrengo sahihi hivyo naamini Kongamano hili la wana AGREST mtajadili namna bora ya kutoka katika mzunguko huu ili Tanzania na Afrika kwa ujumla ziweze kunufaika katika biashara ya mazao na bidhaa za chakula” alisema Pinda.

Aliongeza kuwa Serikali ya CCM inayoongozwa na Rais John Magufuli ina nia njema kabisa ya kuhakikisha kuwa Tanzania inashirikiana na wadau wote katika kuhakikisha Kilimo kinaendelea na kuondoa changamoto zinazojitokeza lakini lazima wajue kwamba Serikali pekee haiwezi kuziondoa bila wataalamu kushirikiana na Serikali.

“ Nikipongeze Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kupitia wataalamu wake wabobevu na mahiri Kwani tunashuhudia kazi zinazofanywa na nanyi na Taasisi zingine katika kukuza shughuli za utafiti na ubunifu hapa nchini” alipongeza Pinda.

Awali akizungumza kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi katibu wa chama hicho Dkt. Betty Waized  alisema kuwa lengo kuu la AGREST ni kusaidia kuchochea maendeleo na matumizi ya Elimu ya Uchumi Kilimo na biashara nchini Tanzania na mikutano hiyo ndio njia mojawapo ya kufikia lengo hilo ni kupitia mikutano hiyo ya kisayansi ambayo wanajadili na kubadilishana mambo muhimu ya uchumi kilimo na kusambaza kwa jamii kubwa zaidi.

Alisema mkutano huu wa 12 kisayansi wa AGREST ni fursa nzuri ya maandalizi ya mijadala  mkutano wa Mifumo ya chakula unaotarajiwa kufanyika mwaka 2021 ambao unalenga kuboresha mbinu za mifumo ya hakika hapa nchini.

“ Tanzania imeingia kwenye uchumi wa kati na  lengo ni ifikapo mwaka 2025 tunahitaji kampuni za kibiashara za kushindana ambazo zitakazofanya kazi kibunifu kwa mifumo ya chakula ambayo inafanya kazi kwa wote” alisema Dkt. Waized.

Alibainisha kuwa mkutano huo wa kisayansi pamoja na mambo mengine unalenga kujibu maswali ya aina gani ya mifumo ya sera inahitajika kusukuma mfumo endelevu wa chakula kwenye bara letu hasa Tanzania.

Katibu huyo wa AGERST alisema mkutano huo umevutia washiriki 80 kutoka sehemu mbalimbali za Tanzania wakiwakilisha wanataaluma, watafiti, maafisa wa Serikali, mashirika yasiyo ya kiserikali na washiriki binafsi ambapo zaidi ya tafiti za kisayansi 30 zitawasilishwa.

“ Mkutano huu pia unawapa nafasi  wanasayansi  wachanga kupata uzoefu namna ya kuandaa na kuwasilisha tafiti zao za kisayansi” alisema Waized.

Katika mkutano huo wanachama hao walimpatia Pinda zawadi mbalimbali ikiwemo Kinyago cha mnyama Tembo pamoja vitenge kwa ajili yake na mke wake lakini pia AGREST walitoa zawadi kwa mwana AGREST mkongwe kwenye chama chao zawadi ambayo ilikwenda kwa Profesa, Aida Isinika kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA).


Reply, Reply All or Forward

Tuesday, December 1, 2020

MBUNGE WA BUYUNGU ATOA MSAADA WA MABATI 300 KUSAIDIA SHULE ZA SEKONDARI

 Mbunge wa Jimbo la Buyungu mkoani Kigoma kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Aloyce Kamamba (katikati kushoto), akikabidhi bati moja kati ya 300 kwa ajili ya ujenzi wa shule za sekondari jimboni humo.
Mkuu wa wilaya ya Kakonko, Kanali Hosea Ndagala (kushoto) akikabidhiwa mifuko ya saruji 100 na Kampuni ya Ujenzi ya Nyanza Road kwa ajili ya ujenzi wa Shule ya Sekondari Kanyonza
Moja ya madarasa ya shule za sekondari jimboni humo.




 Na Mwandishi Wetu, Kigoma.


MBUNGE  wa Jimbo la Buyungu mkoani Kigoma kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Aloyce Kamamba, amekabidhi mabati 300 yenye thamani ya sh.milioni 9 ikiwa ni utekelezaji wa ahadi yake aliyoitoa wakati wa kampeni.

Akizungumza katika hafla ya kukabidhi mabati hayo, Kamamba alisema ni utekelezaji wa ahadi yake aliyoitoa wakati wa kampeni ya kutatua changamoto mbalimbali.

"Niliahidi kutatua changamoto mbalimbali za wananchi katika jimbo letu na nimeanza na changamoto za miundombinu kwa kununua mabati  300 kwa ajili ya ujenzi wa shule zetu" alisema Kamamba.

Alisema mabati hayo yatapelekwa kujenga miundombinu katika shule tatu za sekondari katika jimbo hilo.

Alizitaja shule hizo kuwa ni Sekondari ya  Kanyonza iliyopo Kata ya Kanyonza ambayo itaipata mabati 100, Shule ya Sekondari Kakonko ambayo nayo itaipata mabati 100 na Shule ya Sekondari ya Ushindi iliyopo Kata ya Kasuga.


Mkuu wa wilaya ya Kakonko, Kanali Hosea Ndagala akikabidhiwa mifuko ya saruji 100 na Kampuni ya Ujenzi ya Nyanza Road kwa ajili ya ujenzi wa Shule ya Sekondari Kanyonza ikiwa ni maandarizi ya kupokea  wanafunzi wapya wa kidato cha kwanza  Januari 2021 aliushukuru uongozi wa kampuni hiyo na kumpongeza mbunge huyo kwa kuanza kwa kasi kutekeleza ilani ya uchaguzi ya chamsingi hicho ya 2020/ 2025.

"Nikupongeze mheshimiwa mbunge kwa kuanza kutekeleza ilani ya chama chetu na sisi kama Serikali tutakupa ushirikiano wa kutosha" alisema.

Mwananchi wa Kata ya Kasanda, Alexander Madebwa amemshukuru mbunge huyo kwa juhudi za maendeleo alizoanza kuzifanya hasa katika kuboresha miundombinu upande wa elimu.

Mkazi wa Kata ya Kanyoza  Shetiel Juma amempongeza mbunge wao kwa hatua hiyo aliyoianza ambayo inaleta natumaini mapya kwa wananchi wa jimbo hilo.

Katibu wa CCM Wilaya ya Kakonko, Abdul Kambuga Amempongeza  mbunge huyo kwa kuanza kwa kasi utekelezaji wa Ilani ya chama hicho na kuwa kasi hiyo inawafanya wananchi kuwa na imani na Serikali inayoongozwa na chama hicho chini ya Rais Dkt.John Magufuli.

Monday, November 30, 2020

KANISA LA MORAVIAN WATAKIWA KUTORIDHIKA NA MAENDELEO WALIONAYO

Mwenyekiti na Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Moravian Jimbo la Kusini Mchungaji, Yona Mwambeta, akihubiri Jumapili wakati akiongoza harambee kwa ajili ya ujenzi wa Kanisa la Moraviani Usharika wa Kijichi jijini Dar es Salaam.
Waumini wa kanisa hilo wakiwa katika ibada hiyo.
Ibada ikiendelea.
Ibada ikiendelea.
Mwenyekiti na Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Moravian Jimbo la Kusini Mchungaji, Yona Mwambeta (kushoto) na Mchungaji wa kanisa hilo Usharika wa Kijichi, Raphael Mwampagatwa wakiwa kwenye ibada hiyo.
Maombi yakiendelea.
Harambee ikiendelea. Kushoto ni mke wa Mwenyekiti na Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Moravian Jimbo la Kusini Mchungaji, Yona Mwambeta, Mchungaji Lilian Mwambeta akihesabu sh.550.000 walizotoa kama mchango wao wa ujenzi wa kanisa hilo.
Mchungaji Lilian Mwambeta, akimkabidhi fedha hizo Mwenyekiti wa harambe hiyo, Subilaga Mwambeta.
Waumini wa kanisa hilo na wachungaji wao wakiwa nje baada ya kuhitimisha harambee hiyo.


Na Dotto Mwaibale


MWENYEKITI na Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Moravian Jimbo la Kusini,  Mchungaji, Yona Mwambeta amelitaka kanisa hilo kutoridhika na badala yake waige makanisa mengine yaliyopiga hatua ya maendeleo kwa kujenga makanisa makubwa na kuanzisha miradi ya maendeleo nchini.

Mwambeta aliyasema hayo Jumapili wakati akiongoza harambee kwa ajili ya ujenzi wa Kanisa la Moraviani Usharika wa Kijichi jijini Dar es Salaam.

"Wamoravian tangu siku nyingi wao ni watu wa kuridhika na vitu vidogo nawaambieni badilikeni na kuiga wanavyofanya wenzetu wa makanisa mengine ambao wapo mbali kimaendeleo" alisema Mwambeta.

Alisema kazi ya ujenzi wa kanisa hilo si ya waumini wa kanisa hilo pekee bali ni ya Mungu hivyo uchache wao usiwakatishe tamaa ya kupata fedha za kujenga kanisa hilo.

Akitolea mfano kanisa la Itungi lililopo wilaya ya Kyela mkoani Mbeya alisema lilianza kujengwa na watu wachache lakini leo hii limekuwa ni kanisa la mfano.

Mwambeta aliwataka waumini hao wa Kanisa la Moravian Kijichi kujenga kanisa kubwa litakalo akisi miaka  100 ijayo bila kujali litachukua muda gani kukamilika ujenzi wake.

Aidha Mwambeta aliwataka waumini wa kanisa hilo kuwashirikisha watu mbalimbali bila ya kujali dini zao na madhehebu wanayotoka ili kulijenga kanisa la usharika huo.

Mwenyekiti wa ujenzi wa kanisa hilo Jackson Mwaisemba alisema harambee hiyo ni ya pili  na kuwa wataendelea kufanya nyingine ili kufikia malengo ya kupata sh.milioni 100 zitakazo saidia kuanza ujenzi wa kanisa  hilo.

Mchungaji wa kanisa hilo Usharika wa Kijichi, Raphael Mwampagatwa alimshukuru Mwambeta kwa kuendesha harambee na kuwapa ari na moto mpya waumini wa kuchangia ujenzi huo.

Mchungaji Mwampagatwa alitumia harambee hiyo kutoa namba ya Voda 5312023 na Tigo 0679-607003 kwa ajili ya makanisa mbalimbali, taasisi, mashirika, wafanya biashara na mtu yeyote ambaye atapenda kuchangia ujenzi wa kanisa hilo kiasi chochote cha fedha awe Dar es Salaam na maeneo mengine ndani na nje ya Tanzania na Mungu atawabariki.

Katika harambee hiyo fedha taslimu zilizopatikana zilikuwa ni sh.3,717,000, ahadi sh.4,685,000 na jumla ikiwa ni sh. 8,402,000.

Saturday, November 28, 2020

MTATURU AANZA KUTEKELEZA AHADI ZA WANANCHI KWA KASI YA 4G

Wachungaji na waumini wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Kiaskofu Msalaba Mrefu mjini Singida, wakiwa na pikipiki walizokabidhiwa hivi karibuni na Mbunge wa Singida Mashariki, Miraji Mtaturu kwa ajili ya kazi za kanisa hilo,
Mbunge wa Singida Mashariki, Miraji Mtaturu, akimkabidhi pikipiki, Mkuu wa Jimbo la Kusini Usharika wa Issuna, Mchungaji, Obedi Msele.
Mbunge wa Singida Mashariki, Miraji Mtaturu, akimkabidhi pikipiki, Mchungaji Joyce Madadi wa Usharika wa Ikungi.

 Mbunge wa Singida Mashariki, Miraji Mtaturu, akimkabidhi pikipiki, Mchungaji, Felix Kibiriti.


Na Dotto Mwaibale, Singida.


MBUNGE wa Singida Mashariki, Miraji Mtaturu ameanza kutekeleza ahadi zake kwa wananchi kwa kasi ya 4G.

Mtaturu ametekeleza ahadi yake  kwa kutoa pikipiki tano kwa Usharika wa Kiaskofu Msalaba Mrefu mjini Singida ambazo alimkabidhi Mchungaji Felix Kibiriti kwa niaba ya Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Kati Dkt. Alex Mkumbo kwa ajili ya matumizi ya shughuli mbalimbali za kanisa hilo mkoani Singida.

Mbali ya kukabidhi pikipiki hizo zenye thamani ya sh.milioni 11, Mtaturu pia alimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Ikungi, Edward Mpogolo pikipiki mbili zenye thamani ya sh.milioni 4.6 kwa ajili ya Kituo cha Polisi cha Wilaya hiyo ili ziweze kusaidia kwa kazi.

Akizungumza hivi karibuni katika hafla ya kukabidhi pikipiki hizo Mtaturu alisema utoaji wa pikipiki hizo ni kutimiza ahadi yake aliyoitoa kusaidia kanisa hilo kupata usafiri wa uhakika kwa watumishi wake wanapo kwenda kuhubiri neno la Mungu.

 "Nitaendelea kutimiza ahadi zangu na kushirikiana na wananchi kwa kasi ili kuunga mkono jitihada ya Rais Dkt. John Magufuli ya kutekeleza miradi ya maendeleo" alisema Mtaturu.

Aidha Mtaturu alisema kuwa pikipiki hizo zitatumika katika sharika za Mang'onyi, Issuna, Mungaa na Ikungi zilizopo Jimbo la Singida Mashariki.

 Mtaturu alitoa ahadi hiyo Novemba 8, 2020 wakati akizindua kitabu cha Misemo na Methali za Wanyaturu kilichoandikwa na Mchungaji Dkt.Syprian Yohana Hilinti (PhD) kilichozinduliwa katika Kanisa Kuu la Kiinjili la  Kilutheri Tanzania (KKKT) Singida mjini na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwepo Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt.Rehema Nchimbi huko mshereheshaji katika hafla ya  uzinduzi wa kitabu hicho akiwa ni Mbunge wa Iramba  Mwigulu Nchemba.