Friday, September 9, 2022

UJENZI WA MIRADI YA MAENDELEO HALMASHAURI YA IKUNGI YASHIKA KASI

Muonekano wa baadhi ya majengo ya Kituo cha Afya cha Kata ya Ntuntu ambayo yanaendelea kujengwa. 

Thursday, September 8, 2022

MRADI WA USAID AFYA YANGU NORTHERN WAIPIGA TAFU SEKTA YA AFYA SINGIDA KWA KUTOA MAGARI YENYE THAMANI YA SH.MILIONI 91


Katibu Tawala Mkoa wa Singida Dorothy Mwaluko (katikati) akikata utepe kuashiria upokeaji wa magari mawili yaliyotolewa na Shirika la la Elizabeth Glaser Pediatic Aids Foundation (EGPAF) kupitia Mradi wa USAID Afya Yangu Northern  yenye thamani ya zaidi ya Milioni 91.9 kwa ajili ya kusaidia usimamizi na ufuatiliaji wa huduma za afya mkoani hapa. Kutoka kulia ni Mkurugenzi wa Utafiti wa shirika hilo, Dk. Fredrick Haraka,  Mkurugenzi Mkazi wa shirika hilo, Dk. Sajida Kimambo, Mganga Mkuu Mkoa wa Singida, Victorina Ludovick na Mkururgenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni Melkzedeki Humbe

Furaha ikitawala wakati wa hafla hiyo.


Katibu Tawala Mkoa wa Singida, Dorothy Mwaluko akijaribu kuendesha gari baada ya kukabidhiwa.
Mkururgenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni Melkzedeki Humbe, akijaribu kuendesha gari baada ya kukabidhiwa.
Mkurugenzi Mkazi wa shirika hilo, Dk. Sajida Kimambo, akitoa taarifa ya shirika hilo.
Taarifa ya utendaji kazi ya shirika hilo ikitolewa kabla ya makabidhiano ya magari hayo.
Utambulisho ukifanyika.
Viongozi wa shirika hilo wakisiliza taarifa ya shirika hilo.
Mkurugenzi wa Utafiti wa shirika hilo, Dk. Fredrick Haraka, akijitambulisha.
Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Shirika hilo, Martin Mfikwa akijitambulisha.
Mkurugenzi Msaidizi wa Uendeshaji wa shirika hilo,Jacquesdol Masawe akijitambulisha.
Wajumbe mbalimbali wakisikiliza taarifa kabla ya hafla ya kukabidhi magari hayo.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Singida, Victorina Ludovick akizungumza.
Taswira kabla ya kukabidhi magari hayo.

Tuesday, September 6, 2022

HALMASHAURI WILAYA YA IKUNGI YABAINI MBINU MPYA UKUSANYAJI WA MAPATO

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi, Ally Mwanga akizungumza na Madiwani wa halmashauri hiyo wakati akifungua kikao cha kawaida cha baraza la madiwani ambacho ni cha mwisho wa mwaka kilichoketi leo Septemba 6, 2022 wilayani humo. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa halmashauri hiyo Petro  Mtyana na kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Justice Kijazi.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi, Justice Kijazi akizungumza kwenye kikao hicho.
Kikao kikiendelea. Kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Kamati ya Huduma ya Jamii, ambaye ni Diwani wa Kata ya Siuyu, Selestine Yunde, Mwenyekiti wa Kamati ya Fedha na Uchumi, Halima Ng'imba na Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili, Diwani wa Kata ya Muhintiri, Hamisi Mpuma.
Makamu Mwenyekiti wa halmashauri hiyo Petro  Mtyana akizungumza kwenye kikao hicho.
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Ikungi Mika Likakapa akizungumza kwenye kikao hicho.
Baadhi ya maafisa watendaji na wataalamu wa halmashauri hiyo wakiwa kwenye kikao hicho.

Sunday, September 4, 2022

MABARAZA YA KATA NCHINI YAONDOLEWA UWEZO WA KUSIKILIZA MASHAURI YA ARDHI

Mwenyekiti wa Baraza la Ardhi Wilaya ya Singida, Bahati Colex (kulia) akizungumza katika semina ya wenyeviti wa mabaraza ya Kata wa Manispaa ya Singida iliyohusu mabadiliko ya sheria ya mahakama za utatuzi wa migogoro ya ardhi iliyofanyika jana Septemba 3, 2022 ukumbi mdogo wa baraza hilo mjini hapa. Kushoto ni Mwanasheria wa Manispaa ya Singida, Burton Mahenge ambaye alikuwa mgeni rasmi na mmoja wa wawezeshaji wa semina hiyo.
Mwanasheria wa Manispaa ya Singida, Burton Mahenge ambaye alikuwa mgeni rasmi akioa mada kwenye semina hiyo.
Mshiriki wa Semina hiyo, Saidi Siri Saidi akisisitiza jambo.

Saturday, September 3, 2022

SERIKALI YAWAHAKIKISHIA WAWEKEZAJI MAZINGIRA MAZURI NCHINI

 Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki (wa tatu kutoka kulia) akikata utepe kuashiria  ishara ya uzinduzi wa shamba la uzalishaji kuku wazazi lililopo kwenye Wilaya ya Siha mkoani Kilimanjaro katikahafla iliyofanyika jana Septemba 2, 2022.

Friday, September 2, 2022

Thursday, September 1, 2022

WATOTO 360,000 KUPEWA CHANJO KUJIKINGA NA UGONJWA YA POLIO MKOA WA SINGIDA

Mkuu wa Wilaya ya  Ikungi, Jerry Muro, akiwa amempakata mtoto Harry Nickoson wakati akipatiwa chanjo ya Polio wakati wa uzinduzi wa kampeni ya utoaji wa chanjo ya matone awamu ya tatu dhidi ya ugonjwa wa polio  ambapo kimkoa uliofanyika katika Halamshauri ya Wilaya ya Ikungi mkoani Singida leo hii. Mhe. Muro alimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba katika uzinduzi huo.
Mkuu wa Wilaya ya  Ikungi, Jerry Muro, akikata utepe kuashia uzinduzi wa chanjo hiyo. Kutoka kushoto ni Afisa Elimu Msingi , Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi, Margaret Kapolesya ambaye alimwakilisha Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo katika uzinduzi huo na kulia ni mama wa mtoto Harry Nickoson ambaye alipatiwa chanjo kwa niaba ya watoto wengine wakati akiwa amembeba mwanaye huyo.

Mganga Mkuu wa Wilaya ya Ikungi, Solomon Michaelakizungumza kwenye uzinduzi huo.

Afisa Elimu Msingi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi, Margaret Kapolesya, akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo.

Mratibu wa Chanjo Mkoa wa Singida, Habibu Mwinory akitoa taarifa fupi kuhusu maandalizi ya chanjo hiyo.

Mkuu wa Wilaya ya  Ikungi, Jerry Muro, akiwa amempakata mtoto Giann Kapian Madondola wakati akipatiwa chanjo ya Polio wakati wa uzinduzi wa kampeni ya utoaji wa chanjo ya matone awamu ya tatu dhidi ya ugonjwa wa polio kwa nyumba kwa nyumba. Kulia anayeshuhudia tukio hilo ni Mama wa mtoto huyo, Zawadi Mlugu.
Waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali wakiwa tayari kuchukua taarifa hiyo.
Zulfa Ramadhani akiwa amempakata mtoto wake,Greyson Anatory akisubiri kupatiwa chanjo hiyo.
Wakina mama wakiwa wamewapakata watoto wao wakisubiri kupatiwa chanjo.
Uzinduzi wa chanjo hiyo awamu ya tatu ukifanyika.
Wakina mama wakisubiri watoto wao wapate chanjo.
Wakina mama wakiwa kwenye uzinduzi wa chanjo hiyo.
Uzinduzi wa chanjo ukiendelea.
Uzinduzi wa Chanjo ukiendelea.Kutoka kulia ni Afisa  kutoka Idara ya chanjo Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Happy Saiguran na kushoto ni  Jadili Muhanginonya kutoka katika ofisi hiyo.

Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Jerry Muro akiwa amembeba mtoto aliyepatiwa chanjo hiyo katika uzinduzi huo.
Picha ya pamoja baada ya kufanyika uzinduzi huo.


Na Dotto Mwaibale, IKUNGI

 

MKOA wa Singida unatarajia kutoa chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa polio kwa watoto 363,315 katika kampeni ya awamu ya tatu wenye umri chini ya miaka mitano ili kujikinga na maradhi hayo.

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba katika hotuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Mkuu wa Wilaya ya  Ikungi, Jerry Muro, alisema hayo leo katika uzinduzi wa kampeni ya utoaji wa chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa polio  kimkoa uliofanyika katika Halamshauri ya Wilaya ya Ikungi.

Serukamba alisema katika chanjo hiyo ambayo imeanza kutolewa leo Septemba Mosi itafanyika hadi 4 Septemba na kuagiza kila halmashauri ya mkoa huu kuhakikisha inawafikia walengwa wake wa chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa Polio.

 Alitoa mchanganuo kuwa  katika kampeni hiyo ambayo itakuwa ni ya awamu ya tatu, wilaya ya Iramba inatarajiwa kuwafikia watoto 56,360 ,Wilaya ya Singida vijijini watoto 58,197, Manyoni 45,416 Manispaa ya Singida watoto 39,841, Wilaya ya Ikungi  77,638, Wilaya ya Mkalama watoto 51,658 na Itigi watoto 34,205.

Alisema kauli mbiu ya kampeni hiyo ni "Kila tone la chanjo ya Polio litawekwa Tanzania salama dhidi ya Ugonjwa wa kupooza" ambapo kupitia kampeni hiyo inategemewa watoto wote wenye umri wa chini ya miaka mitano watapatiwa.

Serukalmba alisema kuanza kutolewa kwa chanjo hiyo  kunafuatia Shirika la Afya Duniani (WHO) ilipofika 17 Februari 2022  lilitoa taarifa ya uwepo wa mlipuko wa ugonjwa wa Polio (Wild polio Virus) nchini Malawi ambapo  hadi sasa Malawi imeripoti visa viwili toka mlipuko huu utangazwe mwezi huo.

Aidha, nchi ya Msumbiji imeripoti visa vinne (4) ambapo kisa cha kwanza nchini humo kiliripotiwa mwezi Mei, 2022.

Alisema kufuatia kuonekana kwa ugonjwa huo wa Polio katika Ukanda wa Kusini mwa Afrika, WHO ilitoa tamko kuwa Ugonjwa wa Polio ni janga la Kimataifa (Public Health Emergence of International Concern).

Mkuu huyo wa mkoa alisema tamko hilo la WHO lilikuwa na maana kuwa kugundulika kwa mtoto mmoja mwenye ugonjwa huu kuna uwezekano wa uwepo wa watoto zaidi ya mia mbili wenye maambukizi na uwezo wa kuambukiza watoto wengine na hata watu wazima ambao hawajapata chanjo.

"Shirika la Afya Duniani (WHO) linaelekeza kuwa unapotokea mlipuko au tishio la mlipuko wa ugonjwa wa Polio nchini, nchi husika na nchi jirani zinapaswa kufanya Kampeni ya kutoa chanjo kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano (5) kwa awamu nne mfululizo ili kila mtoto aweze kupata kinga kamili," alisema Serukamba.  

Aliongeza kuwa kufuatia mlipuko wa ugonjwa huu katika nchi za Malawi na Msumbiji, na kwa kuzingatia ukaribu wa kijiografia na mwingiliano wa watu kati ya Tanzania, Malawi na Msumbiji kwa shughuli za kiuchumi na kijamii, kuna uwezekano mkubwa wa maambukizi ya Ugonjwa wa Polio kusambaa na kuingia nchini.

Serukamba alisema ili kuweza kudhibiti ugonjwa huu usiingie nchini na kwa kuzingatia Mwongozo wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Serikali kupitia Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais TAMISEMI na Wadau wa huduma za chanjo nchini inatekeleza Kampeni ya kutoa Chanjo ya Polio kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano. 

"Awamu ya kwanza ya kampeni ilifanyika 24 hadi 27 Machi 2022 na ilitekelezwa katika mikoa minne inayopakana jirani na nchi ya Malawi ambayo ni Mbeya, Songwe, Njombe na Ruvuma. Kampeni hii ililenga kuwafikia watoto 975,839 wenye umri chini ya miaka mitano, na kufanikiwa kuwafikia watoto 1,130,261 sawa na asilimia 115 ya walengwa wote," alisema Serukamba.

Alisema katika  awamu ya pili ya Kampeni hii ilifanyika nchi nzima kuanzia tarehe 18 hadi 21 Mei, 2022 ikilenga kuwafikia Watoto 290, 485  wenye umri chini ya miaka mitano, na kufanikiwa kuwafikia watoto 363,315 sawa na asilimia 125 ya walengwa wote ndani ya Mkoa wa Singida.

"Mkoa wa Singida unawapongeza na kuwashukuru Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri, Wataalamu wa Afya, Mashirika ya Kitaifa na Kimataifa, Vyombo vya Habari na wananchi kwa kufanikisha vyema utekelezaji wa Kampeni hii kwa awamu ya kwanza na ya pili," alisema.