Saturday, August 20, 2022

MBUNGE MTATURU AUNGA JITIHADA ZA RAIS SAMIA ZA KUHAMASISHA SENSA KWA KUANDAA BONANZA

Mbunge  wa Jimbo la Singida Mashariki, Miraji Mtaturu, akizungumza na wachezaji wa Timu za Wakala FC, Sokoni FC na waamuzi wa mpira wakati akifungua bonanza la michezo aliloliandaa kwa ajili ya kuhamasisha Sensa ya Watu na Makazi itakayofanyika Agosti 23, 2022.linaloendelea Viwanja vya Shule ya Sekondari ya Ikungi mkoani Singida ambapo kilele chake kitakuwa kesho.
Mbunge  wa Jimbo la Singida Mashariki, Miraji Mtaturu,  akipiga mpira kuashiria ufunguzi wa bonaza hilo.
Wachezaji wa Timu ya Wakala FC wakiwa katika picha ya pamoja kabla ya kuanza mchezo dhidi ya Sokoni FC. Katika mchezo huo Sokoni FC ilishinda kwa mabao 4-0.
Wachezaji wa Timu ya Sokoni FC wakiwa katika picha ya pamoja kabla ya kuanza mchezo dhidi ya Wakala  FC. Katika mchezo huo Sokoni FC ilishinda kwa mabao 4-0.
Mbunge Mtaturu akifuatilia mchezo dhidi ya Wakala FC na Sokoni FC.
Washariki wakifuatilia mchezo huo.
Mbunge Mtaturu akizungumza na wachezaji wa Timu ya Sokoni wakati akiikagua timu hiyo kabla ya mchezo wao dhidhi ya Wakala FC.
Mbunge Mtaturu akisalimiana na waamuzi wa mchezo huo.
Waamuzi wa mchezo huo wakiwa tayari kwa kazi.Kutoka kulia ni Rehema Dafi, Emanuel Safari na Enock Ayubu.
Mashabiki wakifuatilia mchezo huo. Wa pili kushoto ni Mtangazaji wa mchezo huo, Robert Onesmo kutoka Radio Standard FM ya Mkoa wa Singida.
Washiriki wakiendelea kushuhudia mchezo.
Mwamuzi wa pembeni wa mchezo huoRehema Dafi akiwajibika.

Thursday, August 18, 2022

MASHINDANO TEMBO CUP 2022 YATIKISA ITIGI-TIMU ZA KITARAK FC, DOROTO FC, SANJARANDA FC NA MUHANGA FC ZAINGIA NUSU FAINALI

Diwani wa Kata ya Ipande,Edmon Mpondo (wa kwanza  kushoto) akiwa na wachezaji wa Timu ya Muhanga FC wakati wa mashindano hayo .

Wachezaji wa Timu ya Sanjaranda FC wakiwa katika picha ya pamoja kabla ya kuanza kwa mchezo wa nusu fainali.
Heka heka Uwanjani zikiendelea wakati wa mashindano hayo.

KARDINALI PENGO ABARIKI NA KUFUNGUA MAJENGO YA HOSPITALI YA MAKIUNGU, RC SINGIDA ATOA NENO

 Askofu Mstaafu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo akizungumza wakati wa hafla ya kubariki na kufungua majengo mapya ya Hospitali Teule ya Makiungu inayoendeshwa kwa ushirikiano kati ya Kanisa Katoliki Jimbo la Singida na Serikali. Hafla hiyo ilifanyika sanjari na Misa Takatifu ya ufunguzi wa majengo hayo na kuwaombea wagonjwa.
Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Singida Mhashamu Edward Mapunda akizungumza katika hafla hiyo.
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe.Peter Serukamba akitoa hutuba yake kwenye hafla hiyo.
 Askofu Mstaafu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo (kulia) akiwa na Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbola Singida Mhashamu Edward Mapunda wakati wa misa hiyo.

Wednesday, August 17, 2022

RC SINGIDA AWAKUMBUSHA VIONGOZI, WANANCHI KUHUSU UMAKINI ZOEZI LA SENSA

Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba akizungumza na viongozi mbalimbali wa mkoa huo wakati akifungua kongamano la siku moja la Sensa ya Watu na Makazi lililofanyika Ukumbi wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) Kampasi ya Singida leo hii Agosti 17, 2022.

Katibu Tawala Mkoa wa Singida, Dorothy Mwaluko akizungumza kwenye kongamano hilo wakati akimkaribisha mkuu wa mkoa ili kuzungumza na viongozi hao.
Mratibu wa Sensa ya Watu na Makazi Mkoa wa Singida, Naing'oya Kipuyo akitoa taarifa fupi kuhusu maandalizi ya sensa.
Kongamano likiendelea.

Tuesday, August 16, 2022

TANZANIA YAFIKISHA MAWASILIANO YA INTANETI YENYE KASI MLIMA KILIMANJARO


Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Nnauye akikata utepe kuashiria kuzindua Huduma za Mawasiliano ya Intaneti kupitia Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano katika kituo cha Horombo kilichopo katika Mlima Kilimanjaro jana Agosti 16, 2022. Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Mhandisi Peter Ulanga na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Mohammed Khamis Abdulla (wa nne kutoka kushoto)

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Nnauye akishiriki mkutano kupitia njia ya video na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. John Mongela baada ya kuzindua Huduma za Mawasiliano ya Intaneti kupitia Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano katika kituo cha Horombo kilichopo katika Mlima Kilimanjaro.


 Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Nnauye akizungumza wakati wa hafla ya Uzinduzi wa Huduma za Mawasiliano ya Intaneti kupitia Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano katika kituo cha Horombo kilichopo katika Mlima Kilimanjaro jana Agosti 16, 2022.


 Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Nnauye akisisitiza jambo wakati wa uzinduzi huo.

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Nnauye akizungumza na wadau mbalimbali mara baada ya kuwasili Horombo Hut kwa ajili ya kuzindua huduma za Mawasiliano ya Intaneti yaliyofikishwa katika Mlima kilimanjaro na Shirika la TTCL

RC SINGIDA AWATAKA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA KUFANYA KAZI KWA WELEDI

Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba alizungumza na makarani na wasimamizi wa Sensa ya Watu na Makazi ambao wanaendelea na mafunzo katika Shule ya Sekondari ya Mwenge mjini Singida.Kulia ni  Mratibu wa Sensa ya Watu na Makazi Mkoa wa Singida,Naing’oya Kipuyo na kushoto ni Mratibu wa Sensa Wilaya ya Singida, Mkuki Zephania.
Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba akisisitiza jambo wakati akizungumza na makarani hao.
Mratibu wa Sensa ya Watu na Makazi Mkoa wa Singida,Naing’oya Kipuyo akizungumza katika mkutano huo na Mkuu wa Mkoa.
Makarani na Wasimamizi wa Sensa ya Watu na Makazi wakimsikiliza mkuu wa mkoa (hayupo pichani) wakati wa mkutano huo.
Mkutano huo ukiendelea.
Mwakilishi wa makarani na wasimamizi hao wa Sensa Nembulisi Stephano akitoa neno la shukurani baada ya mkuu wa mkoa kuzungumza nao.

Monday, August 15, 2022

MAANDALIZI JUBILEI MIAKA 50 SINGIDA YASHIKA KASI

Timu ya Mapadri wa Jimbo Katoliki Singida ikiwa kwenye picha ya pamoja muda mfupi kabla ya mchezo wao wa soka dhidi ya Walei jimboni humo. Mchezo huo ulilenga kutoa hamasa na kuchagiza upendo, furaha na amani kama maandalizi kuelekea kilele cha sherehe za Jubilei ya miaka 50 ya Jimbo Katoliki Singida ifikapo Agosti 21 mwaka huu.
 Timu ya Walei Jimbo Katoliki la Singida kabla ya mechi yao dhidi ya mapadri jimboni humo hivi karibuni.
 Timu ya Masista wakivuta kamba dhidi ya Wakinamama Wakatoliki Tanazania jimboni humo (WAWATA) katika tamasha la michezo kuelekea kilele cha Jubilei.