Tuesday, April 9, 2024

MSD YAKUTANA NA WADAU WAKE KANDA YA IRINGA, RC RUVUMA ATAKA WELEDI SEKTA YA AFYA

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali. Ahmed Abbas Ahmed (kushoto) akipokea tuzo maalumu kutoka kwa Mkurugenzi wa Ugavi na Uendeshaji wa Bohari ya Dawa (MSD), Victor Sungusia wakati wa mkutano mkuu wa MSD na  wadau wake wa Mkoa wa Ruvuma uliofanyika Aprili 8, 2024, 

Na Mwandishi Wetu, Ruvuma

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma Kanali. Ahmed Abbas Ahmed, amewataka watumishi wa sekta ya afya Mkoani Ruvuma, kuzingatia weledi na kutoa huduma bora kwa wananchi, ili kuakisi maboresho na uwekezaji mkubwa uliofanywa kwenye sekta ya afya, chini ya uongozi wa serikali ya awamu ya sita.

Kanali Ahmed amesisitiza kuwa, serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan imetoa fedha nyingi kwa ajili ya maboresho na ujenzi wa miundombinu ya afya mathalani majengo, ununuzi wa bidhaa za afya

 na kuwezesha ajira za kutosha,  lengo likiwa kuinua hadhi ya huduma zinazotolewa nchini, hasa zinazomgusa mtanzania wa kawaida.

Kanali Ahmed ametoa rai hiyo hii leo, wakati wa akifungua kikao kazi baina ya MSD Kanda ya Iringa na wadau wake kutoka halmashauri saba za mkoa wa Ruvuma (Madaba Tc, Madaba Dc, Songea MC, Songea DC, Nyasa DC, Mbinga TC na Mbinga DC), kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ruwiko, ulioko Manispaa ya mji wa Songea.

Mkuu huyo wa Mkoa amewakumbusha viongozi hao wa sekta ya afya Mkoani humo, kufanya maoteo yao ya bidhaa za afya kwa usahihi, umakini na kwa wakati ili kuiwezesha Bohari ya Dawa (MSD) kutekeleza majukumu yake ya ugavi wa bidhaa za afya kwa weledi.

Mhe. Ahmed amewataka pia watendaji hao kusimamia ukusanyaji wa mapato, na kutumia vyema vyanzo vyao vingine vya mapato katika kulipa madeni ya MSD, huku akiwakumbusha pia kuhakiki taarifa sahihihi za utunzaji na utoaji wa bidhaa za afya, ili kuepuka upotevu wa bidhaa hizo.

Katika hatua nyigine, Mkuu huyo wa mkoa ameipongeza MSD kwa utendaji wake katika kuboresha hali ya upatikanaji wa bidhaa za afya, huku akiwapongeza kwa kuitisha mkutano huo wa wadau kwani utasaidia kuboresha mahusiano na mawasiliano.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Ugavi na uendeshaji wa MSD Victor Sungusia, amebainisha maboresho mbalimbali yanayoendelea kufanywa na MSD katika nyanja mbalimbali kupitia majukumu yake makuu ya uzalishaji, ununuzi, utunzaji na usambazaji.

Bw. Sungusia amebainisha jinsi MSD ilivyojizatiti katika utekelezaji wa majukumu yake kupitia mifumo ya kisasa ya kidigitali, ugatuzi wa majukumu ya Kanda, ujenzi wa viwanda mbalimbali vya dawa na vifaa tiba, maboresho ya mfumo wa usambazaji wa bidhaa, upanuzi wa maeneo ya uhifadhi na kuwajengea uwezo watumishi wake.

Naye Meneja wa MSD Kanda ya Iringa Bw. Robert Lugembe akiwakiribisha wajumbe wa kikao hicho, alibainnisha kuongezeka kwa uwezo wa MSD kuwahudumia wateja wake na kukidhi mahitaji, sambamba na maboresho ya upatikanaji wa bidhaa za afya mathalani vifaa tiba, mkoani humo.Meneja wa MSD Kanda ya Iringa Bw. Robert Lugembe akizungumza kwenye mkutano huo.

Wadau wa MSD wakiwa kwenye mkutano huo.
Mkutano ukiendelea.
Wadau wa MSD wakiwa kwenye mkutano huo.
Picha ya pamoja na viongozi.
Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali. Ahmed Abbas Ahmed  akiwakabidhi vyeti wadau wa MSD kwa kutambua mchango wao.
Picha ya pamoja na viongozi waliohudhuria mkutano huo.
Vyeti vikiendelea kutolewa.
Vyeti vikiendelea kukabidhiwa kwa wadau wa MSD.
Vyeti vikiendelea kukabidhiwa kwa wadau wa MSD.

Friday, March 22, 2024

WADAU WA MSD WAHIMIZWA KUSIMAMIA MATUMIZI SAHIHI YA TAKWIMU BIDHAA ZA AFYA

Mkuu wa Wilaya ya Masasi Lauteri Kanoni,  akifungua kikao cha wadau na wateja wa Bohari ya Dawa (MSD),  Kanda ya Mtwara Machi 22, 2024.

...........................

Na Mwandishi Wetu, Mtwara

WADAU wa Afya wa Bohari ya Dawa  (MSD) Kanda ya  Mtwara wamehimizwa kusimamia matumizi sahihi ya takwimu za mnyororo wa ugavi wa bidhaa za afya, ili ziwawezeshe kufanya maamuzi sahihi juu ya bidhaa hizo katika maeneo yao.

Akifungua kikao cha wadau na wateja wa MSD kanda ya Mtwara, Mkuu wa Wilaya ya Masasi Lauteri Kanoni amesema uwepo wa takwimu sahihi unaiwezesha MSD kuagiza kwa usahihi bidhaa za afya na kuboresha upatikanaji wa bidhaa hizo kwenye vituo vya kutolea huduma za afya.

Aidha, amewashauri MSD kuhakikisha utaratibu wa vikao  vya mwaka vya wadau ni muhimu kwa pande zote mbili, yaani Bohari ya Dawa (MSD) yenyewe na wadau ili kwa pamoja kuboresha upatikanaji wa bidhaa za afya, kwa kujadili changamoto na kuzitafutia utatuzi.

Kwa upande wake Meneja wa MSD Kanda ya Mtwara Tea Malay ameeleza kuwa kwa sasa kanda ya MSD Mtwara inahudumia vituo vya kutolea huduma za afya 631, na inasambaza bidhaa za afya kila baada miezi miwili.

Naye Meneja Huduma kwa Wateja na Miradi Dkt. Pamella Sawa ameeleza kuwa vikao vya MSD na wadau wake kuanzia sasa vitakuwa endelevu kila mwaka.

MSD Kanda ya Mtwara inahudumia mikoa ya Lindi,Mtwara na Wilaya ya Tunduru.Meneja wa MSD Kanda ya Mtwara Tea Malay, akizungumza kwenye kikao hicho

Wadau wa MSD wakiwa kwenye kikao hicho.
Kikao kikiendelea.
Wadau wa MSD Kanda ya Mtwara wakifuatilia mada kwenye kikao hicho.
Taswira ya kikao hicho.
 

Sunday, March 17, 2024

UBALOZI WA UHOLANZI, SERIKALI WAZINDUA KITABU CHA MWONGOZO WA ULIMAJI VIAZI

Kansela wa kilimo wa Ubalozi wa Uholanzi nchini , Bw Bart Pauwels (mwanzo kulia)pamoja na anayemfuata mwenye miwani ni Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kudhibiti ubora wa Mbegu Tanzania (TOSCI) Dr Patrick Ngwediagi na Balozi wa Uholanzi hapa nchini , Wiebede Boer katikati na kulia kwa Balozi ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Mpango wa Kuendeleza Kilimo Kusini mwa Tanzania (SAGCOT) Bw , Geoffrey Kirenga na mwisho Bw Bob Shuma mdau wa kilimo wakionyesha kitabu cha mwongozo wa kilimo cha viazi ambacho kilizunduliwa.

...................................... 

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

TANZANIA kwa kushirikiana na Ubalozi wa Uholanzi wamezindua kitabu cha mwongozo wa usajili wa aina za mbegu za viazi kwa lengo la kuimarisha ustawi wa kilimo cha viazi na usalama wa chakula hapa nchini.

Akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa kitabu hicho wiki iliyopita jijini Dar es Salaam,Balozi wa Ufalme wa Uholanzi hapa nchini, Wiebe de Boer aliwaambia viongozi waalikwa na wageni mbalimbali kuwa hiyo ilikuwa hatua kubwa katika safari yao ya kuimarisha sekta na kilimo cha viazi hapa nchini.

"Safari ambayo imechangiwa na ushirikiano wa miaka kumi kati ya Tanzania na Uholanzi,katika kipindi cha miaka kumi iliyopita, ushirikiano huu umewavutia wakulima wa viazi wa Uholanzi kusajili aina zao za viazi nchini Tanzania," aliongeza.

Alisisitiza kwamba si hivyo tu bali pia kuvutia uwekezaji kuongeza na kupanua mnyororo wa thamani wa viazi na sasa wanatambua kwamba viazi kama chakula kikuu cha kuhakikisha usalama wa chakula, kuzalisha kipato kwa wakulima na kutengeneza fursa za ajira.

Balozi Boer alisema kuwa ufanisi na tija katika kilimo cha viazi unahitaji matumizi ya mbegubora sambamba na kanuni bora za kilimo zilizochochea ukuaji wa sekta ya kilimo.

Alisema nchini Uholanzi kuna aina zaidi ya 250 za viazi zinazolimwa kwa matumizi mbalimbali,ikiwa ni pamoja na kuchemsha, kukaanga, krisps, kuoka, kuzalisha mbegu na usindikaji wa wanga.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kudhibiti Ubora wa Mbegu Tanzania(TOSCI), Dk Patrick Ngwediagi alisema kitabu hicho kitatumika kama mwongozo kwa wagunduzi wa mbegu za viazi , wakulima na wawekezaji wa ndani na nje ya nchini wanaovutiwa kuwekeza kwenye sekta ya viazi hapa nchini.

"Kwa kweli leo ni hatua muhimu kwa sababu kitabu hiki kitasaidia wakulima kuwa na taarifa za kutosha kuhusu sera, sheria zinazosimamia sekta ya kilimo pamoja na kuangalia changamoto na fursa zilizopo nchini kwenye kilimo cha viazi," alisistiza Dr Ngwediagi.

Dk Ngwediagi alisema kuwa kitabu hicho kitawapa wakulima na wagunduzi hatua kwa hatuajinsi ya kusajili mbegu zao nchini na mchakato wa kuzalisha mbegu bora ili kuhakikisha ukuaji wa sekta hiyo.

“Jinsi hizi zote ni taratibu za hapa nchini katika kuimarisha ukuaji wa sekta na mbegu zote lazima zisajiliwe kwenye Daftari la Taifa la mbegu katika juhudi za serikali kuimarisha usalama wa vyakula kwa watanzania,” aliongeza.

Mshauri wa Kilimo wa Ubalozi wa Uholanzi, Bart Pauwels alisema kuwa Ubalozi wa Uholanzi hpa nchini utaendelea kufanya kazi kwa karibu na Serikali ya Tanzania, Mashirika Yasiyo ya Kiserikali na sekta binafsi kwa ujumla ili kuhakikisha inakuza ukuaji wa sekta ya viazi.

“Kilimo bora ni injini ya ukuaji wa sekta, Ubalozi wa Uholanzi utaendelea kutoa msaada wasekta hii kwa kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika kuboresha kilimo kwa kuleta piateknoloji na ujuzi mwingine wa kitaalamu,” aliongeza.

Kwa miaka 10 sasa, Tanzania na Uholanzi zimekuwa na ushirikiano mzuri katika sekta ya viazi.Kupitia ushirikiano huu, jumla ya aina 16 za viazi zilisajiliwa na kati ya hizo 12 ni aina za Kiholanzi zinazotoa mavuno mengi, kustahimili ukame na wadudu.

Maendeleo haya yalivutia biashara zaidi kwenye mnyororo wa viazi kutoka kwa ufugaji, kukua hadi usindikaji. Ili kusaidia sekta hii zaidi, Ubalozi uliiwezesha TOSCI kutoa mwongozo wa hatua kwa hatua kuhusu taratibu za kuchukua iwapo mwekezaji anataka kusajili aina ya viazi nchini Tanzania kwa ajili ya biashara. Kitabu hiki kimeidhinishwa na TOSCI kwa matumizi ya Tanzania.

ujumbe wa wafugaji 30 wa viazi vya Uholanzi, watafiti, wakulima wanaojihusisha na uendelezaji wa aina za viazi hivyo wametembelea Tanzania. Lengo ni kufahamiana na mahitaji ya soko, upendeleo na kupokea maoni kutoka kwa wakulima. Taarifa hizi zitatumika katikautafiti na ukuzaji wa aina mpya kwa Tanzania.

Saturday, March 16, 2024

MAAFISA WATENDAJI WATAKIWA AJENDA YAO KUWA ANWANI ZA MAKAZI, KUHAKIKI TAARIFA ZA WANANCHI

Mtaalamu wa Mfumo wa Anwani za Makazi kutoka Wizara ya Habari Mawasiliano na Teknolojia ya Habari (WHMTH), Innocent Jacob akizungumza wakati wa siku ya pili ya mafunzo ya siku 14 kwa watendaji wa kata, mitaa, wenyeviti wa Serikali za mitaa na vijiji yanayohusu namna ya kukusanya taarifa za Anwani za Makazi  Manispaa ya Singida.

.........................

Na Dotto Mwaibale, (Singidani Blog)

MAAFISA Watendaji wa Mitaa kote nchini wametakiwa katika vikao vyao vyote vya msingi ajenda yao kubwa iwe ni anwani za makazi pamoja na uhakiki wa taarifa za wananchi.

Ombi hilo limetolewa Machi 15, 2024 na Mtaalamu wa Mfumo wa Anwani za Makazi kutoka Wizara ya Habari Mawasiliano na Teknolojia ya Habari (WHMTH), Innocent Jacob wakati wa siku ya pili ya mafunzo ya siku 14 kwa watendaji wa kata, mitaa, wenyeviti wa Serikali za mitaa na vijiji yanayohusu namna ya kukusanya taarifa za Anwani za Makazi Manispaa ya Singida yaliyoanza Machi 14, 2024 ambayo yameandaliwa na wizara hiyo kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na kuwa siku mbili kati ya hizo 14 zitatumika kwa ajili ya kuhakiki taarifa.  .

Jacob alisema lengo la mafunzo hayo ni kuwawzesha wenyeviti hao ili waweze kutoa taarifa kwa wanananchi za zoezi hilo ndani ya siku hizo na wananchi nao waweze kutoa za kwao kama NIDA, namba ya simu, Tin namba ya biashara na taarifa nyingine za majengo, makazi kama walivyoelekezwa watendaji wa mitaa jinsi ya kulifanya zoezi hilo.

"Watendaji wa mitaa ndio watakao kwenda kukusanya taarifa hizi kwa wakazi wao kwa sababu katika maeneo yote ya utawala wao ndio wahusika wakubwa na watashirikiana na wenyeviti wa mitaa kufanya kazi hiyo," alisema Jacob.

Alisema Wizara ya Habari Mawasiliano na Teknolojia ya Habari (WHMTH), kwa kushirikiana na TAMISEMI, wameandaa zoezi hilo kwa lengo la kuhakiki taarifa za makazi kwa awamu ya pili baada ya awali kufanyika kwa njia ya operesheni ambapo huenda kuna baadhi ya wakazi hawakuweza kupata fursa ya kuingia katika kanzidata ya Anwani za Makazi.

Alitaja baadhi ya vitu ambavyo viliweza kusahulika kuwekwa kwenye kanzidata kuwa ni taarifa ya majengo, viwanja, majina katika vibao vya mitaa hivyo kurudiwa tena katika zoezi hilo la awamu ya pili la uhakiki.

Jacob alisema umuhimu wa Anwani za Makazi zitarahisisha utambuzi kwa wakazi wa eneo husika na kuweza kupata huduma mbalimbali kwa kufikiwa kiurahisi mahala walipo kwa kutumia programu tumizi kwa ajili ya umma inayoitwa NAPA ambayo inapakuliwa kupitia simu janja ambapo wananchi wote hapa nchini wakiwemo wa Manispaa ya Singida wataweza kuingia katika mfumo huo kwa kuandika NAPA Tanzania.

Alisema mafunzo hayo yanafanyika Manispaa ya Kigoma, Iringa na Singida na yatakuwa endelevu kwa kufanyika katika mikoa mingine.

Kwa upande wa Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Singida, Dkt. Adrianus Kalekezi alisema katika mafunzo hayo wataalamu wanaelekeza namna ya kuingiza taarifa katika mfumo wa Anwani za Makazi na kuwa hivi sasa wanauhisha taarifa za awali baada ya kazi hiyo kufanyika awamu ya kwanza.

Dkt. Kalekezi alisema suala hilo la Anwani za Makazi ni la muhimu katika manispaa hiyo kwani wananchi watapata huduma kwa urahisi na alitumia nafasi hiyo kuwaomba wananchi kuilinda miundombinu ya Anwani za Makazi iliyowekwa kama vibao vinavyoonesha majina ya mitaa na barabara na kueleza kuwa ni lazima ilindwe ili waweze kunufaika na zoezi hilo kwani bila miundombinu hiyo inakuwa vigumu kwao kuelekezwa na kuitambua mitaa na barabara.  

Afisa Mtendaji wa Kata ya Mwankoko, Habiba Juma akizungumza kwa niaba ya washiriki wa mafunzo hayo alisema zoezi hilo litawarahisishia kutoa huduma kwa wananchi na kupunguza gharama ya fedha na muda kutoka sehemu moja kwenda nyingine na wananchi wataweza kupata huduma kupitia anuani za makazi.Mtaalamu wa Mfumo wa Anwani za Makazi kutoka WHMTH, George Leonard, akitoa mafunzo kwa watendaji hao.Mtaalamu wa Mfumo wa Anwani za Makazi kutoka WHMTH, Janeth Peter , akiwajibika wakati wa  mafunzo hayo.Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Singida, Dkt. Adrianus Kalekezi, akizungumzia zoezi hilo.

Afisa Mtendaji wa Kata ya Mwankoko, Habiba Juma akizungumzia umuhimu wa mafunzo hayo.
Wataalamu wa mfumo wa Anwani za Makazi wakiwa kwenye mafunzo hayo. Kushoto ni Mtaalamu wa Mfumo wa Anwani za Makazi kutoka Wizara ya Habari Mawasiliano na Teknolojia ya Habari (WHMTH), Innocent Jacob na aliyekuwa Katibu wa Kamati ya Ufatiliaji Operesheni Anwani za Makazi Mkoa wa Singida ambaye pia ni Afisa TEHAMA, Athumani Simba. .
Mwenyekiti wa Wenyeviti wa Serikali za Mitaa Manispaa ya Singida, Abdillai Hussein akimshuru Rais Samia kwa kuwezesha mafunzo hayo kupitia wizara hiyo.
Washiriki wakiwa kwenye mafunzo hayo.
Mafunzo yakiendelea.
Mafunzo yakiendelea.

Attachments area Preview YouTube video MAAFISA WATENDAJI WATAKIWA AJENDA YAO KUWA ANWANI ZA MAKAZI

Wednesday, March 13, 2024

SINGIDA HAWAPO TAYARI KUWA DAMPO LA DAWA, VIFAA TIBA VISIVYO BORA

Katibu Tawala Msaidizi wa Huduma za Uchumi na Uzalishaji Mkoa wa Singida, Stanslaus Choaji ambaye alikuwa mgeni rasmi akifungua mafunzo hayo.

...........................

Na Dotto Mwaibale, (Singidani Blog)

MKOA wa Singida hautakuwa tayari kuwa dampo la matumizi ya dawa, vitendanishi na vifaa tiba ambavyo havina havina ubora.

Katibu Tawala Msaidizi wa Huduma za Uchumi na Uzalishaji Mkoa wa Singida, Stanslaus Choaji aliyasema hayo Machi 12, 2024 wakati akifungua mafunzo ya siku mbili ya wataalamu, wakaguzi na wafamasia wa Halmashauri za wilaya ambao wanakagua dawa, vifaa tiba na vitendanishi yaliyoandaliwa na Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba Tanzania (TMDA)

 Choaji alisema jukumu la Serikali ni kuhakikisha wananchi wote wanapata huduma bora za afya na kuweza kushiriki kikamilifu katika shughuli za uzalishaji mali na kukuza uchumi wa Taifa.

"Hilo ni jukumu kubwa la Serikali na mtaona jinsi inavyofanya kila jitihada kadili itakavyowezekana kwa kutumia rasilimali mbalimbali ili kuwawezesha na kuona wananchi wanapata huduma bora za afya," alisema Choaji.

Alisema kutokana na jitihada hizo zinazofanywa na Serikali wakaguzi hao na watendaji kwenye eneo lao wanaweza kuonesha jinsi ambavyo wanashiriki kwenye hizo jitihada za Serikali kwa kutekeleza majukumu hayo kama vile inavyotakiwa.

Choaji alisema majukumu ya wataalamu hao ni ya msingi kwa sababu yanahusisha maisha ya binadamu hivyo kutekeleza jukumu hilo la kusaidia binadamu ni  kutekeleza jukumu la Mungu aliye tuumba.

Alisema kutenda tofauti na majukumu hayo na kuhakikisha dawa, vifaa tiba na vitendanishi vinavyotumika na binadamu ni kwenda kinyume kabisa na kusudio la Mungu la kumuumba binadamu na mifugo ambayo nayo ni viumbe hai.

Aliwaomba kufanya kaguzi zao kwa kuzingatia kanuni na maadili kwa lengo la kulinda afya za jamii  na kuwahakikishi uwepo wa bidhaa salama

"Tusingependa sisi Mkoa wa Singida tuwe na changamoto ya matumizi ya vifaa hivyo ambavyo havina sifa," alisema Choaji.

Kwa upande wake Meneja wa TMDA Kanda ya Kati, Sonia Mkumbwa alisema kazi yao kubwa ni kuhakikisha wanalinda afya ya jamii kwa kuhakikisha bidhaa za dawa, vifaa tiba na vitendanishi ni bora salama na zenye ufanisi.

Alisema ili jukumu hilo liweze kutekelezeka kwa kuzingatia ukubwa na upana wa nchi yetu yenye halmashauri za wilaya na   mikoa mingi takribani 26 kwa upande wa Tanzania Bara TDMA kwa kuzingatia uchache wa watumishi wake waliona haitakuwa rahisi kufika kila kona ya nchi ndipo kanuni ya kukasimu baadhi ya majukumu na madaraka ya TMDA iliandaliwa na kupitishwa ili majukumu hayo yaweze kukasimiwa kwa halmashauri za wilaya.

Alisema majukumu hayo yamepelekwa katika halmashauri  hizo ili ziweze kusaidia kufanya baadhi ya majukumu ya TMDA kwa kufanya ukaguzi na kuhakikisha wanafuatilia bidhaa ziwe bora na salama katika soko pia kufanya usajili wa maeneo ya kutolea huduma ambayo yapo chini ya TMDA.

"Leo tumewaalika wakaguzi kutoka halmashauri saba za Mkoa wa Singida tumejumuika kwa pamoja ili tuweze kupeana ABC jinsi ya kufanya kazi hizo ambazo zimekasimiwa katika Mamlaka ya Serikali za Mitaa tupo hapa na wataalamu wakaguzi wa  mifugo, wafamasia, wataalamu wa maabara na dawa na wote hawa wanahusika kwa namna moja ama nyingine kuhakikisha hizo bidhaa zinawafikia walengwa ambao ni wananchi.

Washiriki wa mafunzo hayo Upendo Kiula ambaye ni Mratibu wa Huduma za Maabara kutoka Wilaya ya Itigi na Alfred Rwamtoga Mfamasia kutoka Wilaya ya Manyoni wamesema mafunzo hayo yatawasaidia kwani yamewajengea uwezo wa kukagua na kutambua bidhaa ambazo hazina ubora.Meneja wa TMDA Kanda ya Kati, Sonia Mkumbwa pamoja na mambo mengine akizungumzia kuhusu baadhi ya majukumu ya TMDA kukasimishwa Mamlaka ya Serikali za Mitaa TAMISEMI.

Meneja wa TMDA Kanda ya Kati, Sonia Mkumbwa akiwaelekeza jambo washiriki wa mafunzo hayo.

Mshiriki wa mafunzo hayo Upendo Kiula ambaye ni Mratibu wa Huduma za Maabara kutoka Wilaya ya Itigi, akizungumzia umuhimu wa mafunzo hayo.

Mshiriki wa mafunzo hayo Alfred Rwamtoga Mfamasia kutoka Wilaya ya Manyoni akizungumza kuhusu mafunzo hayo


Washiriki wakiwa kwenye mafunzo hayo.
Taswira ya mafunzo hayo.

Afisa wa TMDA, Neema Debwe akichukua moja ya matukio wakati wa mafunzo hayo. 

Mafunzo yakiendelea.Picha ya pamoja ya washiriki wa mafunzo hayo na mgeni rasmi